Sunday, 7 July 2013

ZIARA YA MHE RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI NCHINI CHINA


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, na Naibu Waziri wa Biashara wa China Liu Cigui,katika ukumbi wa Mikutano wa World Hotel China,ambapo alifanya mazungumzo na kutiliana saini Makubaliano masuala ya Biashara.

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mw3amamwema Shein,akiangalia kitabu wakati alipotembelea makumbusho ya kihistoria katika Mji wa Beijing  nchini China,katika ziara ya Kiserikali kwa mualiko wa serikali ya Jamhuri ya Watu wa China,(kulia) Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi zake Zanzibar,Bibi Chen Qiman.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi wa Maendeleo Omar Yussuf Mzee,akibadilishana Hati ya saini ya Mikataba ya uhusiano wa biashara na Naibu Waziri wa Biashara wa China Liu Cigui,baada ya kutilianan saini katika ukumbi wa mikutano wa China World Hotel.



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiuliza suala kwa waongozaji na watoa maelezo katika sehemu za kihistoria zenye kumbukumbu nyingi,zinazopelekea wageni wa aina tofauti kutembelea katika mji huo wa Beinjing nchini China.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo wakati alipotembelea sehemu za Kihistoria zilizopo katika mji wa Beijing nchini China kiwa katika ziara ya kiserikali na ujumbe wake.

Pichani inaonekanwa  moja wapo ya Majengo yaliyokuwemo katika Eneo kubwa sana la kumbukumbu za Kihistoria katika Mji wa Beijing,ambapo wananchi wa China wakiwa na ukarimu wa aina yake.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifuatana naMkewe mama mwamamwema Shein,katika viwanja vya Makumbusho ya Kihistoria nchini Nchini China pamoja na  ujumbe waliofuatana nao katika ziara ya kiserikali.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifuatana na ujumbe wake wakitembelea sehemu mbali mbali za  Kihistoria zilizopo katika makumbusho ya Mji wa  Beijing nchini China kiwa katika ziara ya kiserikali.

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mw3amamwema Shein,akiangalia kitabu wakati alipotembelea makumbusho ya kihistoria katika Mji wa Beijing  nchini China,katika ziara ya Kiserikali kwa mualiko wa serikali ya Jamhuri ya Watu wa China,(kulia) Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi zake Zanzibar,Bibi Chen Qiman.

.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu kusoto) pamoja na ujumbe aliofuatana nao akiuliza suala kwa waongozaji na watoa maelezo katika sehemu za kihistoria zenye kumbukumbu nyingi,zinazotembelea na wageni mbali mbali  katika Mji huo wa Beinjing nchini China,akiwa katika ziara ya Kiserikali ya siku saba.


No comments:

Post a Comment