Sunday, 28 July 2013

Mjumbe wa  Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi Balozi Seif Ali Iddi amekemea tabia ya baadhi ya Viongozi wa Chama hicho kuwa na hulka ya kuwatenga Vijana ambao ndio muhimili na wenye nguvu katika kukipigania Chama hicho.







Kauli hiyo aliitoa katika Ukumbi wa Jamuhuri Wete Pemba wakati akizungumza na vijana wa Chama cha Mapinduzi wa kikundi cha Hatudanganyiki mara baada ya kupokea malalamiko yao dhidi ya baadhi ya Viongozi wa Chama hicho Wilaya ya Wete na Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema zipo kasoro ndogo ndogo zinazotofautiana za mawazo zilizopo baina ya Viongozi na Wanachama lakini  haziwezi kuachwa zinaendelea kudhoofisha nguvu za Chama hicho.
Aliwaasa wana CCM hao kujiepusha na mgawanyiko ndani ya chama ambao unaweza kuleta balaa na kitu kinachowakabili hivi sasa  mbele yao ni kuhakikisha wanapanga mikakati katika kuimarisha nguvu ya chama chao kwa ajili ya ushindi wa mwaka 2015.
Alitahadharisha kwamba hitilafu zinazojichomoza baina ya Viongozi na Wanachama wa chama hicho ni vyema zikatatuliwa na kuishia katika Vikao vya halali na kujiepusha na tabia ya kuitana majina ya ajabu ambayo hutoa mwanya wa kudhoofisha chama.
Balozi Seif alielezea kuunga mkono  vijana hao wa CCM wa kundi la hatudanganyiki Kaskazini Pemba kwa ushujaa wao wa kutetea na kuimarisha Chama cha Mapinduzi na Kuuagiza Uongozi wa CCM Wilaya ya Wete pamoja na Mkoa wa Kaskazini Pemba kufuatilia matatizo yanayowakabili Vijana hao na hatimae kuyatatua nay ale wasio na uwezo nayo kuyawasilisha kwa Uongozi wa Juu wa Chama.
“ Mimi kama Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ambae pia nasimamia shughuli za Serikali ya Chama Tawala nitahakikisha baadhi ya matatizo yenu Vijana nayawasilisha kwa Makamu Mwenyekiti wetu wa CCM Zanzibar ili itafutwe mbinu ya kuyatatua “. Alisisitiza Balozi Seif.
Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM aliwapongeza wana CCM Kisiwani Pemba kwa msimamo wao wa kuendelea kukiunga mkono chama hicho.
Alisema Wanachama wa chama hicho Kisiwani humo ni madhubuti kutokana na kutoyumba kwao licha ya mikiki mikiki wanayopambana nayo kutoka kwa kambi ya upinzani hasa katika nyakati za uchaguzi.
“ Ushindi wa Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi Mkuu unategemea sana wana CCM wa upande wa Kisiwa cha Pemba ambao hawatetereki wala kuyumba kutokana na vitisho vya upinzani “. Alisisitiza Balozi Seif.
Balozi Seif aliendelea kufahamisha kwamba nguvu na uhai wa Chama cha Mapinduzi mara zote unategemea jumuiya zake za Wazazi, Vijana na UWT, hivyo  Vijana hao wanapaswa kuelewa kwamba wao ni tegemeo la Chama wakati wote.
Mapema Vijana hao wa CCM wa kikundi cha hatudanganyiki wakiongozwa na Mwenyekiti wao Omar Rashid walielezea changamoto wanazokabiliana nazo kila siku katika harakati zao za kuimarisha Chama Cha Mapinduzi.
Walisema asilimia kubwa ya changa moto hizo ambazo zimo ndani ya uwezo wa Viongozi wenyewe zimekuwa zikiwapa wakati mgumu kutokana na udhaifu binafsi uliopo kwa baadhi ya Viongozi wa CCM Wilaya na Mkoa.
Walieleza kwamba upo ushahidi wa wazi unaoonyesha baadhi ya Viongozi wa CCM Wilaya na Mkoa kufuja mali za Chama kwa maslahi yao binafsi pamoja na kujishirirkisha katika vitendo vya rushwa wakati zinapotokea fursa za ajira kwa ajili ya Vijana hao.
Baadaye Balozi Seif alifika katika Kijiji cha Michakaeni Chake Chake Pemba kuipa pole Familia ya Mwanaharakati wa Chama cha Mapinduzi Marehemu Bibi Fatma Omar Khatib ambae aliyefariki dunia hivi karibuni baada ya kupata ajali ya kugongwa na Gari.
Akiifariji Familia hiyo Balozi Seif aliwataka ndugu na jamaa wa marehemu Bibi Fatma Omar Khatib kuwa na moyo wa subra katika kipindi hichi kigumu cha maombolezo.
Alisema msiba huo wa Bibi Fatma ambao utaendelea kukumbukwa katika kipindi kirefu mbali ya kuiathiri familia hiyo lakini pia umewagusa takriban wana chama wa chama cha mapinduzi wote waliopata taarifa ya msiba huo Zanzibar na bara kwa ujumla.
Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM pia alimtembelea Mzee  mwanaharakati wa CCM wa miaka mingi Kisiwani Pemba Bibi Habiba Ali Hamadi hapo nyumbani kwake Mtaa wa Michakaeni.
Bibi Habiba mwenye umri wa Miaka 70 aliwahi kupata ajali ya gari wakati wa kampeni za mwanzo za uchaguzi wa vyama vingi vya siasa ambapo CCM iliibuka na ushindi kwa kumuwezesha Dr. Salmin Amour kuiongoza  Zanzibar mnamo mwaka 1995.
Balozi Seif alimuahidi Bibi Habiba ambae hadi sasa ni Balozi wa CCM wa nyumba kumbi kwamba Uongozi wa chama cha Mapinduzi utakuwa pamoja na  yeye kwa kumpatia misaada kadri hali itakavyoruhusu kutokana na mchango wake mkubwa aliyoitoa ndani ya chama hicho.
 
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
28/7/2013.
 
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akitoa huduma za vyakula katika futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif pamoja na watendaji wa Wizara yake hapo Nyumbani kwake Mazizini






Watendaji wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wanapaswa kuendeleza tabia waliyokuwa nayo ya kushirikiana pamoja katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi ili kufanikisha lengo lililokusudiwa na Taifa.
Nasaha hizo zimetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya kufutari pamoja na baadhi ya Wafanyakazi hao hapo nyumbani kwake Mazizini nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Futari hiyo pia iliwajumuisha majirani wa Balozi  Seif waliyozunguuka makazi yake, Kamati ya wananchi wanaoishi katika eneo la Uwanja wa ndege pamoja na baadhi ya Wawakilishi na watendaji wa Taasisi nyengine za Serikali.
Balozi Seif alisema ushirikiano wa watendaji wa Wizara hiyo ambao ndio unaosimamia shughuli za Serikali umemuwezesha  yeye akiwa mtendaji mkuu wa shughuli hizo kutekeleza kazi zake kwa ufanisi.
Alieleza kwamba wafanyakazi mara nyingi wanakuwa kazini pamoja kwa kipindi  mrefu katika harakati za za kimaisha za kila siku jambo ambalo wanastahiki kupendana  na kushirikiana kwa vile wanaishi kama familia moja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwapongeza wafanyakazi hao wa Ofisi yake kwa kazi kubwa ya kuandaa bajeti ya Wizara hiyo na hatimae kupitishwa na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika Kikao cha kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara za Serikali kwa mwaka wa Fedha wa               2013 /2014.
Akizungumzia funga ya mwezi mtukufu wa ramadhani  inayoendelea Balozi Seif aliwataka waumini wa Dini ya Kiislamu pamoja na wafanyakazi hao kutekeleza ipasavyo ibada hiyo katika taratibu zilizivyowekwa na Dini.
Alisema Mwezi Mtukufu wa Ramadhani umekuwa kigezo kikubwa kwa waumini wa Dini ya Kiislamu ambao huwafundisha mambo mengi endapo watayaendeleza yatawajengea hatma yao njema ya baadae.
Mapema wakitoa shukrani kwa niaba ya watendaji wa Ofisi hiyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dr. Khalid Salum Mohd wamemshukuru Balozi Seif kwa utaratibu wake wa kuwashirikisha watendaji wake katika futari ya pamoja.
 Walisema tabia hiyo kwa kiasi kukubwa imekuwa ikiendelea kuongeza  upendo baina ya Viongozi na Wafanyakazi  hao sambamba na wale wananchi wanaowahudumia.
“ Hii ni tabia ya upendo kati ya Uongozi na wale wanaowaongoza ambayo hujenga udugu na ushirikiano unaoongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao “. Alifafanua Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Dr. Khalid.
Wakati huo huo Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi alisema Vijana wa Umoja wa Vijana Chipukizi wa CCM ndio tegemezi kubwa katika kuona Taifa la Tanzania linaendelea kuongozwa katika  misingi ya amani na utulivu.
Mama Asha ambae pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kaskazini “B “ alisema hayo wakati akiufungua Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana Chipukizi wa CCM Wilaya ya Kaskazini B uliofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya CCM Jimbo la Kitope iliyopo Kinduni.
Alisema iwapo taifa halitajizatiti katika kuwaanda vijana kwa ajili ya Uongozi wa hapo baadae mifarakano inayoendelea kuandaliwa hivi sasa kwa kisingizio cha dini inaweza kujaleta balaa katika jamii hapo baadae.
Mama Asha alifahamisha kwamba mifarakano hiyo licha ya kwenda kinyume  na maamrisho ya hiyo dini yenyewe lakini pia inapingana na ile azma ya waasisi wa Taifa hili ya kuwaandalia mazingira mazuri ya maamuzi wananchi kwa kuleta ukombozi.
“ Waasisi wetu walipigania kujikomboa na madhila ya wakoloni ambayo baadhi ya watu wanakuwa vibaraka vya kushawishi kurejeshwa  kwa mfumo huo ambao utasababisha kuwanyima wananachi walio wengi uwamuzi wa kujiamulia mambo yao wenyewe “. Alitahadharisha Mjumbne huyo wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Kaskazini “ B “.
Katika kuunga mkono harakati zao Vijana hao wa Chipukizi Mjumbe huyo wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Kaskazini B Mama Asha Suleiman Iddi amechangia Shilingi Milioni 1,000,000/- kwa ajili ya Wajumbe wote 150 wa Mkutano Mkuu wa Chipukizi Wilaya ya Kaskazini B.
Mama Asha pia alikabidhi mchango wa shilingi Laki 200,000/- kwa Kikundi cha Dufu cha Kijiji hicho, Shilingi Laki 200,000/- kwa Kikundi cha maigizo pamoja na kuahidi kutoa sare kwa Wajumbe wote 150 wa Mkutano huo Mkuu wa Chipukizi Wilaya.
Naye kwa upande wake  Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi   alichangia jumla ya shilingi Laki 500,000/- kusaidia kufanikisha Mkutano huo Mkuu wa Vijana wa Chipukizi Wilaya ya Kaskazini “ B”.
Akitoa Taarifa fupi ya Umoja wa Vijana Chipukizi Wilaya ya Kaskazini B Mwenyekiti wa Umoja huo Ali Khamis alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana ndani ya unoja huo kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa kikundi cha kujitolea kilichojikubalisha kunadi ilani ya CCM wakati wote.



Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

27/7/2013.

Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki ya Kati na kati kati mwa Bara la Afrika wa Kampuni  ya Umeme { Elsewedy Electric }ya Nchini Misri  Bwana Mohamed Sakr akimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Azma ya Kampuni yake ya kutaka kuwekeza kiwanda cha kutengeneza Transfoma hapa Zanzibar







Kampuni ya Kimataifa inayojihusisha na masuala ya huduma za Umeme ya Nchini Misri  ya Elesewedy Electric imeonyesha nia ya kutaka kuwekeza kiwanda cha kutengeneza Transfoma pamoja na vifaa mbali mbali vya Umeme hapa Zanzibar.
Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki ya Kati na kati kati mwa Bara la Afrika wa Kampuni hiyo  Bwana Mohamed Sakr alieleza hayo alipokutana kwa mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisini wake Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar.
Bwana Mohamed Sakr alisema Uongozi wa Kampuni hiyo umeridhika na mazingira ya Utulivu na ukarimu uliopo hapa Zanzibar na Kampuni yake kushawishika kutaka kuwekeza vitega uchumi vyake  ili kutoa huduma za Nishati sambamba na kuzalisha soko la ajira kwa Vijana wa Zanzibar.
Alisema Kampuni yao yenye ubora nambari moja Afrika na Mashariki ya kati na Nambari Tano Duniani imekuwa ikitoa huduma za umeme na kufikia hatua za kuongeza Matawi yake katika mataifa mbali mbali Duniani.
Bwana Mohamed aliyataja baadhi ya Mataifa ambayo Kampuni hiyo imeshawekeza miradi yake kuwa ni pamoja na Cameroun,Equitoria Guinea, Kenya na Ethiopia kwa Afrika na Colombia na  Brazil katika Bara la Amerika ya Kusini na Russia iliyopo Barani Asia.
“ Mtazamo wetu ni kuwekeza mradi wa Dola za Kimarekani Milioni 300 Nchini Kenya na Dola za kimarekani Milioni 600 Nchini Ethiopia wakati muelekeo wetu hivi sasa tumelenga kuwekeza hapa Zanzibar “. Alisisitiza Mkurugenzi huyo wa Kanda ya Mashariki ya Kati na kati kati mwa Bara la Afrika wa Kampuni hiyo   ya Elsewed Bwana Mohamed.
Bwana Mohamed alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwamba Kampuni hiyo imepanga kutumia mtaji wa zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni tatu { U$ 3,000,000,000 } kwenye miradi yake katika kipindi kijacho.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliuhakikishia uongozi wa Kampuni hiyo inayojishughulisha na masuala ya huduma za Umeme Nchini Misri kwamba Serikali itajitahidi kuona malengo ya Kampuni hiyo yanafanikiwa ipasavyo.
Balozi Seif alisema hatua hiyo itaongeza nguvu za uwekezaji zilizolengwa na Serikali hapa nchini hatua ambayo itasaidia kupanua wigo wa ajira ambao Serikali pekee hauwezi kuutekeleza.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliuagiza Uongozi wa Kampni hiyo kuharakisha hatua za maombi ya mradi wao ili taasisi zinazosimamia  Nishati, Uwekezaji na Viwanda ziupitie na kutoa mchango wao katika kufanikisha azma ya kuanzishwa mradi huo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.
Wakati huo huo Balozi Seif ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kitope amewakumbusha wazazi wa Kijiji cha Mgonjoni kiliomo ndani ya Jimbo hilo kuwapatia elimu watoto wao ili kuwajengea mazingira bora ya maisha yao hapo baadaye.
Balozi Seif alieleza hayo wakati akisalimiana na Wananchi hao pamoja na kuwapatia futari na nguo wananchi hao wa Mgonjoni  kwa ajili kumudu kuendelea vyema na ibada yao ya funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhani unaoendelea.
Alisema hakuna kitu bora na sahihi cha wazazi hao wanarithisha watoto wao isipokuwa elimu ambayo ndiyo itakayowabadilisha Kiuchumi na kimaendeleo katika Kijiji chao.
“ Kinamama muelewe kwamba mtakuwa na kazi ya ziada katika kuwahimiza watoto wenu kwenda kujipatia elimu “. Alisisitiza Balozi Seif.
Katika kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kijiji cha Monjoni Balozi Seif amechangia Shilingi 1,000,000/- kwa ajili ya ununuzi wa matofali, saruji na fedha za fundi kwa ajili ya ujenzi wa Msikiti wao.
Aliwahakikishia wananchi hao kwamba Uongozi wa Jimbo hilo utaendelea kutafuta mbinu mbali mbali za kutatua matatizo yanayowakabili likiwemo suala la Madrasa na Skuli.
Naye Mke wa Mbunge huyo Mama Asha Suleiman Iddi amewaomba akinamama wa Kijiji hicho kujikusanya pamoja na kuunda kikundi cha ushirika na yeye atakuwa tayari kuwapatia mtaji wa kuendesha shughuli zao za uzalishaji.
Mapema asubuhi Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi alikabidhi vifaa mbali mbali kwa ajili ya uendelezaji wa ujenzi wa Madrasat Mujitahidina iliyopo katika Kijiji cha Kitope Tobora.
Vifaa hivyo ni pamoja na Matofali, Nondo, Mchanga fedha za fundi pamoja na kukipatia chuo hicho Misahafu na Juzuu kwa ajili ya wanafunzi wa Madrasa hiyo.
Akizungumza na Walimu, Wanafunzi na Wazazi wa Kijiji hicho Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha  amewasihi Washirika na wahisani wa ujenzi wa Misikiti Nchini hivi sasa kuelekeza nguvu zao katika ujenzi wa Madrasa za Quran.
Mama Asha alisema Visiwa vya Zanzibar hivi sasa vimepunguza kiu ya Misikiti ambayo baadhi yake imejengwa ikiwa na upungufu wa  waumini jambo ambalo kama nguvu hizo zimetumiwa katika ujenzi wa madrasa ili kupunguza  kero kubwa linaloikabili Jamii la uhaba wa maeneo ya kusomea Quran.
Aliwakumbusha waumini kurejea katika maadili ya zamani ya upendo miongoni mwao ili ile sumu ya chuki, uhasama na matendo mengine maovu wanayofanyiana waumini hao yapungue au kuondoka kabisa.
Alifahamisha kwamba mioyo lazima ibadilike katika njia ya Mwenyezi Muungu ili jamii ipate kufanikiwa katika mambo yao ya kila siku badala ya kuwatumia Walimu na wafanuzi wa madrasa katika matendo maovu ya mifarakano isiyo na hatma njema.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

26/7/2013.

Monday, 8 July 2013

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akikabidhi Seti ya TV Flat Screen kwa Timu ya Soka ya Mwache Alale United




Mbunge wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akikabidhi Seti ya TV Flat Screen kwa Timu ya Soka ya Mwache  Alale United baada ya kuibuka na ushindi wa godi 5 – 3 dhidi ya African Boys ya Upenja kwenye mchezo wa Fainal ya Kombe wa Zaweda.

Pambano hilo lilichezwa katika uwanja wa Kitope na kushuhudiwa na Mbunge huyo Balozi Seif.

Picha no:-984 ni:- Nahodha wa Timu ya Soka ya Mwache Alale Abdullghani Gullan akipokea kikombe kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 5-3 dhidi ya African Boys ya Upenja.

Picha na Hassan Issa wa –OMPR – ZNZ.

Press Release:- { Michezo }:-
Hatimae Timu ya Soka ya Mwacha Alale United imeibuka na ubingwa wa mashindano ya Kombe la Zaweda ndani ya Jimbo la Kitope baada ya kuilaza Timu ya African Coast ya Upenja kwa mabao 5 – 3 yaliyopatikana kwa njia ya Penalti katika pambano la fainali lililochezwa kwenye uwanja wa Kitope.
Pambano hilo lililokuwa na ushindani mkali kwa timu zote mbili lilichezwa kwa dakika 90 bila ya mshindi lilishuhudiwa na wapenzi kadhaa wa mchezo wa soka wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi.
Mabingwa hao wapya wa Kombe la Zaweda Mwache Alale United  walifanikiwa kupata ushindi huo baada ya kufunga Penalti zote tano wakati wapinzani wao African Boys ya Upenja wakapata Penalti tatu na kupoteza moja.
Mgeni rasmi wa pambano hilo Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif alikabidhi zawadi kwa bingwa wa mashindano hayo, mshindi wa pili pamoja  na zawadi kwa  timu zote zilizoshiriki katika mashindano hayo ambayo ni ya pili kufanyika tokea kuanzishwa kwake mwaka uliopita.
Balozi Seif aliwakabidhi mabingwa wa Kombe hilo Mwacha Alale United Seti moja ya TV, King’amuzi chake, shilingi 300,000/- taslimu, seti moja ya jezi, mpira pamoja na Kikombe cha ubingwa.
Mshindi wa Pili African Boys ya Upenja ikakabidhiwa shilingi  laki 150,000/- Taslimu, seti moja ya jezi, pamoja na mpira wakati mshindi wa Tatu Mahonda Kids wakaibuka na Seti moja ya jezi, shilingi 75,000/- taslim pamoja na Mpira.
Mchezaji bora na mdogo kuliko wote katika mashindano hayo alikuwa Said Khamis Kidagaa aliyepata zawadi ya shilingi 20,000/- taslimu na  Mfungaji bora wa mashindano hayo Abdull Nyafu wa African Coast ya Upenja alipata zawadi ya shilingi 20,000/-.
Mchezaji bora wa mashindano hayo Ali Alawi na Golkipa bora Siad Abdulla kutoka Timu ya Zaweda wamepata zawadi ya shilingi 20,000/- taslimu kila mmoja wakati zawadi ya shilingi 50,000/- Taslimu kwa timu bora katika mashindano hayo ilichukuliwa na timu ya soka ya Zaweda.
Muamuzi bora wa mashindano hayo aliibuka Haroun Kuchi aliyefanikiwa kupata zawadi ya shilingi 20,000/- taslim pamoja na mpira mmoja mmoja kwa kila timu ilizoshiriki katika mashindano hayo.
Timu zilizoshiriki mashindano hayo ya Zaweda Cup ni pamoja na Mbuyuni, Fujoni Boys, Mahonda Union, Kitope United,Zaweda, Mgambo F.C, Kilimani City, Kibweni Youth Organization, New Star, Mahonda Kids,washindi wa Pili African Boys ya Upenja na Mabingwa wa mashindano hayo Mwacha Alale United.
Mapema Mbunge huyo wa Jimbo la Kitope Balozi Seif alikabidhi zawadi kwa washindi wa mchezo wa Pete wanawake ambapo bingwa ni watanashati wa Kitope waliopata shilingi laki 100,000/- Taslimu, Mpira  pamoja na Seti ya Jezi.
Mshindi wa pili wa mchezo huo wa netball ni timu ya wanawake ya kiwengwa iliyozawadiwa shilingi laki 100,000/- Taslimu, Mpira na Seti ya Jezi.
Akizunguma mara baada ya pambano hilo la fainal na zawadi Mbunge huyo wa Jimbo la Kitope Balozi Seif aliwakumbusha wana michezo nchini kuendelea kushikamana katika michezo ili kuleta upendo michezoni na ndani ya Jamii.
Balozi Seif aliwatahadharisha wanamichezo hao kuvitumia viwanja vya michezo kwa mnasaba wa kiungwana na ustaarabu na kuacha tabia ya kuvifanya viwanja hivyo kuwa ni maeneo ya kuporomoshwa kwa matusi.
“ Haipendezi kuona maeneo ya viwanja vya michezo nchini yanakuwa sehemu ya kuporomoshwa matusi ambayo mara nyingi huelekezwa kuwakashifu viongozi wanaowaongoza wanamichezo hao “. Aliasa Balozi Seif.
Aliwapongeza Wanamichezo pamoja na uongozi wa Kamati ya mashindano hayo ya Zaweda Cup  kwa juhudi zao zilizosaidia kukamilisha mashindano hayo kwa amani na furaha.
Jumla ya shilingi Milioni 2,700,000/- zimetumika kugharamia vifaa mbali mbali vya mashindano hayo ya Zaweda Cup katika ununuzi wa TV, jezi mipira pamoja na kikombe.
 
 
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
7/7/2013.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibarf Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Wafanyabiashara


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibarf Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Wafanyabiashara ya kushajiisha ushiriki wa Sekta Binafsi katika maadhimisho ya Sherehe za kutimia miaka 50 ya Zanzibar  aliokutana nao hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
 
Press Release:-
Wazanzibari wote walioko ndani na nje ya Zanzibar wana fursa, haki na Uhuru wakati wowote kusaidia kwa njia mbali mbali maandalizi na hatimae  kufanikisha sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 kutimia robo Karne ambayo ni  sawa na miaka 50 iliyopita.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibarf Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Wafanyabiashara ya kushajiisha ushiriki wa Sekta Binafsi katika maadhimisho ya Sherehe za kutimia miaka 50 ya Zanzibar  aliokutana nao hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Balozi Seif alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imelenga kuwaungalisha Wazanzibari wote popote pale walipo ili kuona wanashiriki kikamilifu kwenye maadhimisho hayo yanayotarajiwa kuwa ya aina yake na Kihistoria hapo mwakani.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliieleza Kamati hiyo baadhi ya mambo yaliyopangwa kufanya ndani ya vugu vugu la maadhimisho hayo ambayo yatasaidia kutoa taaluma kwa Jamii hasa kile kizazi kilichozaliwa baada ya mapinduzi ya mwaka 1964 ambacho bado hakijaelewa dhamira hasa ya kufanyika kwa Mapinduzi ya Zanzibar.
Balozi Seif ambae pia ni Mwenyekiti wa Sherehe na Maadhimisho ya Taifa aliyataja baadhi ya mambo yaliyolengwa kufanya katika kipindi hicho cha sherehe kuwa ni pamoja na warsha, makongamano kwa kushirikisha vyama vya Siasa,  matembezi ya kuashiria sherehe hizo pamoja na usiku maalum wa burdani na ngoma za asili.
Alifahamisha kwamba Mnara Maalum wa kumbu kumbu ya Mapinduzi utajengwa ili kupamba sherehe hizo za aina yake zitakazotoa pia fursa ya kualikwa kwa Viongozi wa nchi rafiki za mwanzo zilizojitokeza kuunga mkono mapinduzi ya mwaka 1964.
“ Katika kupamba sherehe zetu tumeandaa kutoa nishani maalum kwa watu waliotoa mchango mkubwa kwa Taifa tokea Mapinduzi ya Mwaka 64 wakiwemo askari wa Vikosi vya ulinzi na usalama, wana sanaa na Utamaduni “. Alisisitiza Mwenyekiti huyo wa Kamati ya sherehe na maadhimisho ya Taifa.
Balozi Seif aliwaomba wajumbe wa Kamati hiyo ya Wafanyabiashara ya kushajiisha ushiriki wa Sekta Binafsi katika maadhimisho ya Sherehe za kutimia miaka 50 ya Zanzibar  kuhakikisha  wanajitolea kwa nguvu zao zote katika kufanikisha vyema kazi waliyopewa na Taifa.
Naye mjumbe wa Kamati hiyo Mbunge wa Jimbo la Mpendae Salum Turky aliahidi akujitolea kugharamia ujenzi wa mnara huo wa kumbu kumbu ya Mapinduzi unaotarajiwa kujengwa katika eneo la Mzunguuko wa Bara bara za makutano ya Nyumba za Maendeleo Michezani.
Aliiomba Kamati ya Sekriterieti ya Sherehe na Maadhimisho ya Taifa Zanzibar kumpatia michoro ya ujenzi wa Mnara huo ili apate wasaa wakujiandaa kuitekeleza kazi hiyo ambayo anaamini kwamba atakuwa ametoa mchango na kuweka historia ndani ya maadhimisho ya sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar.
“ Tunashukuru kuona kwamba Zanzibar inaingia kutimiza miaka hamsini ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 ikiwa katika hali ya amani na utulivu hali ambayo ni nadra kupatikana katika baadhi ya Nchi Duniani “. Alifafanua Mjumbe huyo wa Kamati hiyo Salum Turky.
Kwa upande wao wajumbe wengine Simai Mohd, Ahmada Abdullwakil, Sharifa Khamis na Meneja wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Zantel Zanzibar Mkweche wameipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa uamuzi wake wa kuanza kujiandaa mapema ya sherehe hizo kubwa.
Hata hivyo waliishauri Serikali kufikiria kutenga  maeneo ambayo wafanyabiashara wanaweza kuyatumia kutangaza biashara zao katika njia maalum itakayotoa fursa ya kuchangia maadhimisho hayo.
“ Sio mbaya kwa Serikali kutafuta njia ya kuwashirikisha pia Wafanyabiashara wa Tanzania Bara hasa wale waliowekeza vitega uchumi vyao hapa Zanzibar na pia wenye imani ya muelekeo wa kuunga mkono maadhimisho hayo “. Alisisitiza Simai Mohd.
“ Wakati tumejikubalisha na sisi kuingia katika ulimwengu wa sayansi na tenolojia na kwa vile wenzetu wamejiimarisha vyema katika masuala ya utambulisho wao itapendeza  nasisi kuelekea huko kwa kuwa na utambulisho wetu maalum ambao utawapa fursa wageni na watalii kuielewa vyema Zanzibar“. Alishauri pia Mjumbe mwengine wa kamati hiyo Ahmada Abdull wakil.
Katika kuanza rasmi jukumu zima walilopewa wana kamati hao walifikia uwamuzi  wa kuanza kikao cha dharura mara baada ya mkutano huo kupanga mikakati ya kufanikisha jukumu lao.
Ujumbe wa mwaka huu wa Maadhimisho ya sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar kutimia robo Karne { sawa na miaka 50 } ni  Amani, Umoja na Maendeleo yetu ni Matunda ya Mapinduzi ya 1964. “ Mapinduzi Daima “.
 
 Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
7/7/2013.
 

MAKAMO WA PILI WA RAIS AKITOWA ZAWADI KATIKA JIMBO LA KITOPE






Mbunge wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif akikabidhi Seti ya TV kwa Katibu wa Maskani ya Tupendane iliyopo katika Kijiji cha Kazole Ndugu Machano Haji Machano kutekeleza ahadi alizotoa kwa wana CCM wa maskani hiyo.

Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
 
 
Press Release:-
Wanachama wa CCM na Wananchi wameaswa kujiepusha na tabia ya baadhi ya  watu wenye tabia ya kuendeleza matusi na kejeli kwa viongozi wao ambayo hujenga chuki na uhasama na hatimae kuashiria kuvunjika kwa amani na utulivu hapa Nchini.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha  Mapionduzi Balozi Seif Ali Iddi alitoa nasaha hizo wakati akikabidhi msaada wa seti za Televisheni, Mashine ya DVD na fedha za kuunganishia TV kwa maskani ya CCM ya Tupendane na ile ya Mama Asha Balozi Maskani zilizomo ndani ya Jimbo la Kitope Wilaya ya Kaskazini “ B”.
Balozi Seif ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kitope aliyekuwa akitekeleza ahadi alizozitoa kwenye maskani hizo alisema tabia hizo zinapaswa kutoungwa mkono na Wananchi walioelekeza nguvu zao zaidi katika kujiletea maendeleo yao.
Alifahamisha kwamba Jamii imekuwa  shahidi katika matukio kadhaa yaliyowahi kutokea ndani ya vipindi tofauti hapa Nchini na kuleta uvunjifu wa amani ambayo yameacha makovu baada ya kusababishwa na baadhi ya watu wanaoichezea amani kwa maslahi yao binafsi.
“ Jamii itaendelea kukumbwa na matatizo na kukosa utulivu wa kimaisha endapo Taifa hili halitaongozwa na Chama tawala cha Mapinduzi chenye sera zinazotekelezeka na kukubalika na Wananchi walio wengi “. Alisisitiza Balozi Seif Ali Iddi.
Mbunge huyo wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwakumbusha wana CCM na wananchi wa Jimbo hilo waelekeze nguvu zao katika kujiletea maendeleo na Viongozi wao watakuwa tayari kuunga mkono juhudi hizo.
Aliwashauri wananchi hao na wana ccm kuanzisha vikundi vya ushirika vitakavyosaidia kuongeza nguvu za pamoja katika kuelekea kwenye uzalishaji wa miradi tofauti ya kiuchumi na kupunguza ukali wa maisha.
“ Ni vyema mkaanzisha vikundi vya ushirika vya uzalishaji mali na mimi wakati wote nitakuwa tayari kuvipa nguvu vikundi hivyo ili muweze kutekeleza vyema malengo mliyojipangia ndani ya vikundi hivyo “ . Alifafanua Balozi Seif.
Katika utekelezaji wa ahadi hizo Balozi Seif pia alikabidhi mchango wa shilingi laki tano kwa ajili ya ununuzi wa matofali na saruji ya kuendeleza ujenzi wa Maskani ya Tupendane.
Halkadhalika Balozi Seif akakabidhi seti za jezi na mipira kwa maskani zote mbili za Tupendane na ile ya Mama Asha Balozi Maskani vifaa na vitu vyote hivyo vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 2 na Laki Saba {2,700,000/- }.
 
 
Othaman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
7/7/2013.

Sunday, 7 July 2013

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimia na Rais Barrak Obama wa Marekani baada ya kuwasili nchini Tanzania





Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi atembelea mabanda ya maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya saba saba


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiingia kuatika  mabanda ya maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya saba saba Jijini Dar es salaam akiambatana na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mh. Pandu Ameir Kificho pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed.

Balozi Seif akiangalia sabuni safi ya mapande ya kufulia iliyotengenezwa na Kiwanda cha Star Natural Product chini ya utaalamu wa Shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo { SIDO }.


Mtaalamu wa dawa za asili za miti shamba kutoka Meli Nne Herbal Producti Zanzibar Bibi Salma Othman akimpatia maelezo Balozi Seif juu ya utengenezaji wa biadhaa zao kwa kutumia miti ya asili.
Nyuma ya Balozi ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed na Waziri wa Viwanda na Biashara wa SMT Mh. Abdulla Kigoda.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiangalia viatu vya makubadhi vilivyotengenezwa na Saccos ya Nia Safi Women kutoka chake chake Kisiwani Pemba.

 Msimamizi muandamizi wa mauzo katika banda la vifaa vya mawasiliano vya kampuni ya Sam Sung Bwana Dionis Ezekiel Mboya akimuonyesha balozi Seif teknolojia ya hali ya juu inayopatikana katika seti za Televisheni kwa kutumia ishara ya mkono au kidole bila ya kugusa.


Mwakilishi wa Kampuni ya Poly Machinery Co. LTD kutoka Jamuhuri ya Watu wa China Bwana Even Mao akimpatia maelezo Balozi Seif jinsi ya mashine zilizotengenezwa na kampuni hiyo jinsi zinavyofanya kazi.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
Press Release:-
Shirika la kuhudumia Viwanda vidogo vidogo Nchini Tanzania { SIDO } limepongezwa kwa hatua yake iliyochukuwa ya kuwajengea mazingira bora ya miundo mbinu Wananchi katika upatikanaji wa vitendea kazi vyenye viwango vinavyowawezesha  wakulima Nchini kumudu kuzalisha kitaalamu zaidi.
Pongezi hizo zimetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuyatembelea Mabanda mbali mbali yaliyopo kwenye maonyesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa Jijini Dar es salaam.
Balozi Seif alisema Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo vidogo { SIDO }  limejikita zaidi katika kusaidia jamii hasa wananchi wanaojishughulisha na kilimo jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limeleta faraja na kuelekea kwenye njia ya kumkomboa mwananchi wa kipato cha chini.
Akionyesha furaha yake Balozi Seif alieleza kwamba yapo mambo ya kushangaza katika mabanda ya maonyesho ambayo yamefanywa na wananchi wenyewe wazalendo bila ya kushirikishwa wataalamu wa  nje ya nchi kwa kutumia Teknolojia ya hapa hapa nchini.
  Nimefurahishwa sana kutokana na vitu vingi nilivyovishuhudia katika mabanda haya ya maonyesho niliyoyatembelea. Ukweli halisi  huwezi kufikiria kama bidhaa nilizoziona zimetengenezwa hapa nchini kutokana na ubora wake “. Alisistiza Balozi Seif.
Aliwaomba wajasiri amali mbali mbali wanaoshiriki katika maonyesho hayo kuhakikisha kwamba wanatumia fursawaliyoipata eneo hilo  kutokanana na ushiriki wao kwenye maonyesho hayo kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa zenye  kiwango ili kujijengea soko la uhakika ndani na nje ya Nchi.
Mapema Meneja mauzo wa Shirika la kuhudumia Viwanda  vidogo vidogo           { SIDO } Henric Mdede alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwamba Taasisi yake imekuwa ikitengeneza vifaa tofauti vya uzalishaji kulingana na mahitaji ya wananchi wa kipato cha kawaida.
Alisema utaratibu huo Umekusudiwa  kutoa fursa kubwa zaidi kwa wazalishaji wadogo wadogo hasa wale walioamua kujiunga katika Muungano wa wazalishaji katika mfumo.
Naye mwakilishi wa Kampuni ya Poly Machinery co. LTD kutoka Jamuhuri ya Watu wa China ambayo imeshiriki katika maonyesho hayo ya saba saba Bwana Even Mao alisema Kampuni yao imefikia uwamuzi wa kuwekeza vitega uchumi vyao Nchini Tanzania kutokana na mazingira mazuri yaliyopo.
Bwana Even Mao alisema Tanzania nimebarikiwa kuwa na utajiri mkubwa wa rasilimali ya ardhi ambayo ikitumiwa vyema inaweza kuchangia mapato ya Taifa pamoja na kuimarisha sekta ya kilimo ambayo ndio inayochukuwa asilimia kubwa ya wananchi wake kujishughulisha na Kilimo.
“ Ukweli sisi kampuni yetu tumelazimika kufungua tawi letu hapa kufuatia Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa ni nchi ya kilimo “. Alisikika Bwana Even Mao akitamka maneno hayo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif katika ziara hiyo alifanikiwa kuyatembelea mabanda ya maonyesho ya shirika la kuhudumia Viwanda vidogo vidogo { SIDO }, wajasiri amali wa bidhaa mbali mbali za vyakula vikavu ,viungo, uchongaji pamoja na fani ya ufumaji vya  Bara na Zanzibar.
Nyengine ni vifaa vya kisasa vya mawasiliano vinavyotengenezwa na kampuni ya Sam Sung pamoja na mashine tofauti za kuhudumia bidhaa za kilimo zikiwemo pia zile za kutotolea vifaranga vya kuku na kukobolea vyakula vya nafaka. 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
6/7/2013.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif azindua Kituo cha kutoa huduma cha PBZ katika jengo la Mamlaka ya Mapato Zanzibar


 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akikifungua Kituo cha kutoa huduma cha PBZ sambamba na uzinduzi wa huduma za kusafirisha fedha kwa haraka { World Remit Money Transfer Services } kiliopo kwenye jengo la Mamlaka ya Mapato Zanzibar { ZRB } Mazizini nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.


 Balozi Seif akiangalia ujumbe wa simu aliotumiwa wa kupokea fedha kwa njia ya huduma ya kusafirisha fedha kwa haraka kutoka kwa mmoja wa Marafiki zake Bwana Hassan aliyeko Canada kupitia kituo cha huduma cha PBZ kiliopo Mazizini. Pembeni yake ni  mtendaji wa Kituo hicho cha PBZ Rashid Mohd Hassan akisubiri kuthibitisha ukweli wa Ujumbe huo ili ampatie fedha zake.
Balozi Seif akifurahia fedha alizotumiwa na Rafiki yake Bwana Hassan aliyeko Canada baada ya kuzipokea kupitia Kituo cha PBZ kiliopo Mazizini katika mfumo wa huduma za kusafirisha fedha kwa njia ya haraka.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Limited Nd. Juma Amour Mohammed akitoa taarifa katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha kutoa huduma cha PBZ sambamba na uzinduzi wa huduma za kusafirisha fedha kwa haraka hapo Mazizini.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza katika uzinduzi wa Kituo cha kutoa huduma cha PBZ sambamba na huduma za kusafirisha fedha kwa haraka hapo katika jengo la Mamlaka ya Mapato Zanzibar      { ZRB } Mazizini.Kushoto yake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Watu wa Zanzibar Nd. Abdull-rahman Mwinyi Mbegu na Kulia yake ni Kaimu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo Dr. Mwinyihaji Makame.




Baadhi ya Wafanyakazi wa Benki ya Watu wa Zanzibar walioshuhudia uzinduzi wa Kituo cha kutoa huduma cha PBZ sambamba na huduma za kusafirisha fedha kwa haraka hapo Mazizini.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.


Asilimia 70% ya watu wote Duniani hawana ajira hali ambayo inaongeza umaskini hasa katika Mataifa machanga.


 Rais wa Uganda Yoweri Museveni akiwa pamoja na Baadhi ya washiriki wa Majadiliano ya Kimataifa  ya ushirikiano kwa wote kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.

 Waziri wa Biashara, Vuiwanda na Masoko Zanzibar Ahmed Mazrui akiwa pamoja na  washiriki wenzake wa Majadiliano ya Kimataifa  ya ushirikiano kwa wote kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.


Rais Jakaya Mrisho kikwete wa Tanzania na baadhi ya Viongozi washiriki wa Majadiliano ya Kimataifa  ya ushirikiano kwa wote kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.Kulia yake ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Bw. Joaquim Chisano.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa miongoni mwa washiriki wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa  ya ushirikiano kwa wote kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.


Raia wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikweta akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seiof Ali Iddi wakiwa nje ya ukumbi wa Mwalimu Nyerere wakati wa mapumziko wa Majadiliano ya Kimataifa  ya ushirikiano kwa wote kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
Press Release:-Uimarishwaji wa Miundo mbinu ya Viwanda sambamba na ongezeko kubwa la uzalishaji wa Kilimo ndio njia muwafaka ya kukabiliana na  ukosefu wa ajira unayoyakumba mataifa kadhaa machanga yanayoendelea Duiniani.Hayo yalikuwa mawazo na muelekeo wa baadhi ya Viongozi wa Mataifa kadhaa Duniani walioshiriki kwenye majadiliano ya Kimataifa ya ushirikiano kwa manufaa ya wote ukiwa katika siku ya pili unaofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.Waziri Mkuu  Mstaafu wa Malaysia Dr. Mahathir muhamad aliuambia mkutano huo wa majadiliano ya Kimataifa kwamba asilimia 70% ya watu wote Duniani hawana ajira hali ambayo inaongeza umaskini hasa katika Mataifa machanga.Alieleza kwamba nchi changa zinapaswa kujikita zaidi katika miundo mbinu ya viwanda ambavyo uwepo wake hupunguza wimbi kubwa la wananchi wasiokuwa na ajira.Dr. Mahathir alisema kuna haja kwa mashirika na Taasisi za Kimataifa Duniani kuendelea kuunga mkono msimamo wa Mataifa machanga  katika kunyanyua uchumi kwa lengo la kupunguza hali duni za Kimaisha za Wananchi wa Mataifa hayo.
Alisema Taasisi hizo zina mchango mkubwa katika kusaidia kuongeza nguvu za uzalishaji na hatimae kupunguza kwa kiasi kikubwa umaskini uliokithiri katika nchi zinazoendela kujinasua Kiuchumi.“Msimamo wa Mataifa machanga  wa kunyanyua hali za maisha ya wananchi wake unafaa kuunga mkono na Taassi na Mashirika  binafsi hasa yale ya Kiuchumi ambayo yana mchango mkubwa  katika kusaidia kunyanyua uchumi wa wananchi hao “. Alisisitiza Waziri Mkuu huyo wa Malaysia Dr Mahathir.Akitilia mkazo suala la umuhimu wa Viwanda Rais Yoweri Museveni wa Uganda alisema mataifa machanga ni vyema yakabadilika ili kuelekea kwenye sekta hivyo ambayo ni muhimumi mkuu unaoongeza kasi ya uchumi Duniani.Rais Museveni alieleza kwamba kumekuwa na mivutano na misongamano ya umiliki wa ardhi unaotokana na uwiano wa vipato kwa baadhi ya watu katika mataifa mbali mbali maskini hali ambayo husababisha zaidi umaskini.Alizashauri nchi changa kuhakikisha kwamba zinajinasua katika wimbi la umaskini kwa vile tayari zinajiendesha zenyewe kwa karibu miaka 50 sasa tokea zipate uhuru wake kutoka kwa wakoloni waliokuwa wakihodhi  na kusafirisha rasilmali za nchi hizo.“ Tumekuwa tukishuhudia balaa kubwa kwa baadhi ya mataifa ndani ya bara la afrika wakati wanapofanikiwa kuibua miradi mipya ya kiuchumi hasa inayohusu mafuta na gesi “. Alifafanua Rais Museveni.Wakitoa taarifa za kitafiti , kiuchumi, kijamii na Kisayansi baadhi ya Wataalamu wa Nchi shiriki wa majadiliano hayo ya Kimataifa ya ushirikiano kwa manufaa ya wote walieleza umuhimu wa Mataifa machanga kujenga miundo mbinu ya teknolojia ya Kisasa katika ngazi za chini.Profesa Heneri Dzinotyiweyi wa Zimbabwe alisema mfumo huo utazijengea uwezo na nguvu madhubuti jamii katika muelekeo sahihi wa kuingia ndani ya mfumo wa kisasa wa sayansi na Tekonojia mbwembwe.Naye waziri wa Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mnyaa Mbarawa alisema mawasiliano ya teknolojia yamesaidia kuibadilisha kwa haraka harakati za kila siku za maisha ya jamii.Profesa Mnyaa alitolea mfano wa mawasiliano ya simu ndani ya bara la Afrika yalivyonyanyua uchumi, ustawi wa jamii kupitia mitandao ya simu ambayo mbali ya kutoa huduma za haraka hasa za kifedha pia zimeweza kutoa ajira kwa kundi kubwa la Vijana.“ Utafiti wa hivi karibuni umebainisha kuwa zaidi ya watu Milioni 360,000,000 Barani Afrika hivi sasa wanatumia huduma za mawasiliano ya simu sambamba na huduma za kifedha kupitia mitandano hiyo ya simu “. Alifafanua Profesa Mnyaa.Akiufungua mkutano huo  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alisema umefikia wakati kwa mataifa machanga kuona umuhimu wa kuwekeza katika miundo mbinu ya Sayansi na Teknolojia ya Kiuchumi.Alisema Tanzania tayari imeanza kujiandaa na mfumo huo kwa kuimarisha elimu ya msingi na sekondari hadi chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mandela ambacho kinatarajia kutoa wataalamu wazuri wa fani ya Sayansi na Teknolojia kwa manufaa ya Nchi.Vile vile alielezea kwamba suala la utafiti katika fani hiyo muhimu serikali ya Tanzania imeamua kutenga fedha kwa vijana wenye vipaji maalum katika kuwajengea uwezo zaidi kwa kuwawezesha kuibua  teknolojia ya sayansi itakayoleta nafanikio ya haraka katika Jamii.Alifahamisha kwamba wapo vijana ambao tayari wameanza kuwekeza katika masuala ya sayansi kwa kubuni mashine za kisasa zinazotoa huduma katika taaluma bora inayokwenda na wakati.“ Tatizo linalowakabili wakulima walio wengi nchini Tanzania hivi sasa ni kuendelea na jembe la mkono ambalo limepitwa na wakati kutokana na mabadiliko yaliyopo hivi sasa ya sayansi na teknolojia kwa kuangalia zaidi uchumi “. Alisema Dr. Kikwete.Zaidi ya wajumbe 800 kutoka Nchi mbali mbali Duniani wameshiriki Mkutano huo wa Siku Nne wa Majadiliano ya Kimataifa ya ushirikiano kwa manufaa ya wote.Zanzibar inawakilishwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiambatana na baadhi ya Mawaziri na watendaji wakuu wa Serikali kutoka sekta ya Biashara, fedha na  Utawala. Othman Khamis Ame na Mwantanga Ame.Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
29/6/2013.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akilizindua jengo jipya la madarasa la Skuli ya Msingi ya Miwani ya Jimbo la Uzini.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akilizindua rasmi jengo jipya la madarasa mawili la Skuli ya Msingi ya Miwani iliyomo ndani ya Jimbo la Uzini.

 Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Mohd Raza akimpatia maelezo ya ujenzi wa Jengo la Skuli ya Msingi ya Miwani Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif mara baada ya kulizindua rasmi.

 Balozi Seif akimpongeza Msaidizi Mkurugenzi wa Benki ya Watu wa Zanzibar  { PBZ } Ame Haji Makame kwa hatua ya benki hiyo kusaidia vikalio kwenye jengo jipya la skuli ya msingi ya miwani.Kulia yao ni Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Mohd Raza Hassan na Pembeni yao Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Dr. Islamu Idriss.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akisalimiana ana Wanafunzi wa Skuli ya Msingi wa Miwani waliojaa furaha baada ya kuzinduliwa rasmi kwa jengo lao jipya.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ. Press Release:-Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema  wakati umefika kwa Wananchi kuwa na hadhari katika kuangalia Mtu mwenye muelekeo wa kuwafaa katika kuwasimamia kusukuma mbele maendeleo yao wanayoyahitaji kwenye maeneo yao.Kauli hiyo aliitowa wakati akizindua rasmi jengo jipya na la kisasa la Skuli ya Msingi  ya Miwani ndani ya Jimbo la Uzini lililojengwa ndani ya kipindi cha miezi miwili na Mwakilishi wa Jimbo hilo Mh. Mohd Raza Hassan.Balozi Seif alisema ile tabia ya baadhi ya wananchi kukumbatia watu wanaoendeleza ubinafsi inafaa kupigwa vita kwa hali yoyote ile kwa vile inachangia kuzorotesha kasi ya Maendeleo ya Wananachi.Aliwahimiza Viongozi, washirika na wahisani zikiwemo Taasisi za Kijamii na zile za maendeleo zilizomo katika Halmashauri za Wilaya kujikita zaidi katika kuunga mkono juhudi za Wananachi kwenye sekta za Mendeleo na Kiuchumi wakiangalia zaidi ile sekta muhimu ya Elimu.“ Siku zote tunasema tuwekeze kwenye elimu ambayo watoto wetu itawasaidia wao wenyewe kwa kupata muelekeo na mafanikio ya maisha yao sambamba na kusaidia familia zinazowazunguuka “. Alisisitiza Balozi Seif.Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimpongeza Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Mohd Raza kwa hatua yake aliyochukuwa ya ujenzi wa Jengo hilo la madarasa mawili lililokamilika huduma zote ikiwemo vikalio ambalo limesaidia kuiepusha Skuli ya Miwani kuchukuwa wanafunzi katika mikondo miwili.Balozi Seif alisema juhudi za Mwakilishi huyo ni miongoni mwa utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010 ya CCM pamoja na kukamilisha ahadi alizotowa wakati wa kuomba ridhaa ya kuliongoza Jimbo hilo.Aliwakumbusha Viongozi wengine wa Jimbo, Wilaya na hata mkoa kuunga mkono jitihada za Wananachi wa Miwani katika kukamilisha jengo jengine la Madarasa  Sita la Skuli hiyo ambalo linahitaji nguvu za ziada za Viongozi hao likiwa limekwama kwa  miaka minne sasa.Alisema katika kuunga mkono juhudi hizo za Wananchi ambapo zinahitajika kiasi cha shilingi Milioni Tisa { 9,000,000/- } kukamilisha hatua ya linta ili likabidhiwe  Wizara ya Elimu  na Mafunzo ya Amali kwa Ukamilishaji aliahidi kuchangia Shilingi Milioni Mbili { 2,000,000/- }.“ Sisi viongozi kuanzia Wawakilishi wa kuteuliwa, Mbunge, Madiwani na hata halmashauri za Wilaya tunalazimika kuunga mkono juhudi hizi ili kutowavunja moyo wananchi tunaowaongoza katika Majimbo yetu “. Alikumbusha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.Akitoa salamu za Benki ya Watu wa Zanzibar { PBZ } iliyosaidia Vikalio vyote vya jengo hilo Meza 100 na Viti 100 vyenye thamani ya shilingi Milioni 16,000,000/-  Msaidizi Mkurugenzi Mtendaji wa Benki  hiyo  Ame Haji Makame amesema benki hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi za Wananchi popote pale.Nd. Ame alisema benki ya Watu wa Zanzibar inajali maendeleo ya Jamii na wakati mwengine kushawishika kusaidia miradi yao tofauti ikiwemo zaidi sekta ya elimu ambayo ndio mkombozi wa Taifa lolote.Naye kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bibi Mwanaidi Saleh amempongeza Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Raza kwa juhudi zake za kusaidia nguvu za Wizara hiyo katika ukamilishaji wa majengo  ya Skuli.Bibi Mwanaidi alisema juhudi za Mwakilishi huyo za kukamilisha majengo mawili ya Skuli ndani ya Jimbo hilo limeipunguzia mzigo mkubwa Wizara ya Elimu wa kukamilisha majengo kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na wizara hiyo.Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Elimu amewakumbusha Wananchi katika maeneo mbali mbali Nchini kuhakikisha kwamba majengo ya skuli wanayoyaanzisha yanatengewa vyumba maalum kwa ajili ya vitengo vya Kompyuta.Alisema Wizara imeanzisha mfumo maalum wa mafunzo ya kompyuta kuanzia elimu ya msingi kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi wa Zanzibar kwenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na Teknolojia yaliyopo Duniani.Akitoa shukrani zake katika hafla hiyo ya uzinduzi wa jengo jipya la Skuli ya Miwani iliyomo ndani ya Jimbo la Uzini Mwakilishi wa Jimbo hilo Mh. Mohd Raza Hassan alisema kwamba uwepo wa Viongozi katika Jamii upo kwa ajili ya kusimamia matakwa ya Wananchi.Mh. Raza alisema tabia ya baadhi ya Viongozi kuigonganisha vichwa jamii ni kutowafanyia haki Wananachi wanaowaongoza na hatimae inaviza maendeleo yao na kuwaongezea chuki na fitna baina yao.Mapema katika Risala yao iliyosomwa na Mwalimu  wa Skuli ya Msingi ya Miwani Juma Abdulla wananchi hao wa Kijiji cha Miwani walisema bado wanakabiliwa na changamoto kadhaa ndani ya Kijiji hicho.Mwalimu Juma alizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na ukosefu wa bara bara, mashine za uchapaji , ukosefu wa Daktari katika kituo chao cha Afya pamoja na umaliziaji wa jengo lao la madarasa sita ambalo linaweza kusaidia muendelezo wa mkondo mmoja tu skulini hapo.Jengo jipya  la  madarasa mawili la Skuli ya Msingi ya Miwani litakalokuwa na uwezo wa kuchukuwa wanafunzi 122 ambapo wanafunzi  56 kwa kila chumba  lilijengwa ndani ya kipindi cha miezi miwili kwa gharama za shilingi Milioni 30,000,000/- .Katika hafla hiyo Mwakilishi wa Jimbo la Uzini pia alikabidhi Mchango wa Shilingi Milioni Mbili kwa ajili ya Kusaidia maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 50 ya Mapinduzi Mtukufu ya Zanzibar hapo mwaka 2014.Fedha hizo zitasaidia katika Ofisi ya Mkoa Kusini Unguja, Wilaya ya Kati, Jimbo la Uzini Kichama pamoja na kukabidhi pia mipira kwa ajili ya Timu za Skuli 12 zilizomo ndani ya Jimbo la Uzini. Othman Khamis Ame.Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.26/6/2013.