Monday, 9 September 2013



Uhusiano wa  kubadilishana nyaraka za Kihistoria kati  ya Oman na Zanzibar  unaweza kuwasaidia wananchi  wa pande  mbili  pamoja na watafiti wa masuala ya Kihistoria kuelewa kwa kina maingiliano ya muda mrefu yaliyopo kati ya  Wazanzibar na Waoman ambayo yanafanana  Kisilka na Kiutamaduni.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati wa mazungumzo yake na Ujumbe wa Viongozi sita wa Serikali ya Oman ulioongozwa na Waziri wa Habari wa Nchi hiyo Dr. Abdulmumin Mansour Bin Said Al- Hasani aliokutana nao hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Balozi Seif alisema Zanzibar na Oman zimekuwa na uhusiano wa Kihistoria wa muda mrefu tokea karne ya 18 ambao umethibitishwa na wataalamu pamoja na watafiti wa mambo ya Kihistoria kutoka vyuo vikuu tofauti Duniani.
Alielezea haja kwa Viongozi na Wananchi wa Oman na Zanzibar kuendelea kushikamana na kushirikiana katika masuala mbali mbali ya maendeleo yatakayosaidia ustawi wa vizazi vya sehemu zote mbili rafiki.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliipongeza Serikali ya Oman  kupitia ushirikiano wa mamlaka  ya kumbu kumbu na nyaraka ya Oman na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar { SUZA } kwa kuandaa Kongamano la Kimataifa la Ustaarabu wa Kiiislamu kwa Nchi za Mashariki mwa Bara la Afrika.
Balozi Seif alisema  uamuzi huo wa kufanywa kwa kongamano hilo  hapa Zanzibar umekuja wakati muwafaka kwa wataalamu wa mambo ya Kale kubainisha kwamba  Historia ya Uislamu imeanzia hapa Zanzibar.
“ Nimefurahi kusikia kwamba Historia ya Uislamu imeanza Zanzibar. Inaonyesha watafiti wameliona hili kutokana na asilimia kubwa ya wakaazi wa Visiwa vya zanzibar  kuwa  waumini wa Dini ya Kiislamu sambamba na Utamaduni wake “. Alieleza Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alishauri tafiti za Wataalamu wa masuala ya Historia ambazo zitaibuka katika Kongamano hilo  zielekezwe zaidi kunufaisha wananchi  na waislamu wa ukanda wote wa Afrika Mashariki.
“ Tafiti hizi za Wataalamu wetu wa Kihistoria itapendeza kama zitaendelea kubakishwa katika maktaba zetu ili zisaidie wananchi, waislamu na hata wasomi wetu wa vyuo vikuu vya ukanda wetu wa Afrika Mashariki “. Alisisitiza Balozi Seif Ali Iddi.
Naye Kiongozi wa Ujumbe huo wa Serikali ya Oman Waziri wa Habari wa Nchi hiyo   Dr. Abdulmumin Mansour Bin Said Al- Hasani alisema ipo haja ya kuendelea kuhifadhiwa kwa Historia iliyopo ya Zanzibar na Oman kwa faida ya vizazi vijavyo.
Dr. Abdulmumin alieleza kwamba upeo wa tabia za watu wa oman na Zanzibar unaolingana ndio unaochangia na kushawishi wageni na watalii wa mataifa mbali mbali  duniani  kupendelea kuzitembelea nchi hizi zinazofanana kiutamaduni.
Waziri huyo wa Habari wa Oman alifahamisha kwamba Kongamano  hilo la ustarabu wa Kiislamu linalofanyika hapa Zanzibar  mbali ya utafiti uliopatikana lakini pia litafungua uhusiano katika Nyanja nyengine za maendeleo kwa nchi shiriki.
Dr. Abdulmumin alielezea faraja yake kutokana na umuhimu wa udugu uliopo  kati ya watu wa Oman na Zanzibar ambao umepelekea waoman wengi  kujitokeza kushiriki kwenye kongamano hilo.
Alifahamisha kwamba ipo ishara ya kuendelea kwa ziara za mara kwa mara kati ya watu wa pande hizo mbili.
Kongamano hilo la siku tatu linalofanyika katika Hoteli ya Kimataifa ya La Gemma Della East Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja na kushirikisha Mataifa yapatayo 17 lina lengo la kuitangaza Zanzibar katika Nyanja za utafiti na Taaluma Kimataifa.
Hilo ni kongamano la Pili la Kimataifa la Ustarabu wa Kiislamu  kufanyika likitanguliuwa na lile la mwaka 2012 lililofanyika Nchini Uganda na kutolewa uamuzi wa kongomano linalofuata kufanyika hapa Zanzibar kutokana na  Historia yake  iliyopo  sambamba na uhusiano  wa karibu iliyonayo na Mataifa ya Kiarabu.


Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
3/9/2013.

Mchango mkubwa unaoendelea kutolewa na Jamuhuri ya Uturuki katika kusaidia Sekta ya Afya Zanzibar umesaidia kuipunguzia mzigo mkubwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwahudumia Wananchi wake hasa wale wanaohitaji kusafirisha  kwa ajili ya matibabu zaidi ya kitaalamu nje ya Nchi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo wakati akiwashukuru Madaktari 45 na Maprofesa watano wa Jamuhuri ya Uturuki waliokuwepo Nchini kutoa huduma mbali mbali za afya ikiwemo upasuaji alipozungumza nao katika ukumbi mdogo wa Jumba la Wananchi Forodhani Mjini Zanzibar.
Balozi Seif alisema ziara za kila mwaka kwa timu za madaktari wa Uturuki wanaokuja kujitolea Zanzibar katika sekta ya afya zimeleta faraja na upendo baina ya watu wa Uturuki na Zanzibar hali ambayo alieleza kwamba inapaswa kuimarishwa na kuenziwa zaidi.
Alifahamisha kwamba mpango wa Madaktari hao kupitia taasisi zao za misaada za kutoa msaada wa vyandarua 8,000 pamoja na usomeshwaji wa wazanzibari wapatao 86 tokea kuanza kwa mpango huo mwaka 2007 umetoa picha halisi kwa taasisi hizo jinsi zilivyokubali kujitolea kusaidia huduma za Kibinaadamu hapa Nchini.
“ Tunafurahi kuona kwamba msaada wenu huu wa vyandarua umekuja wakati muwafaka kwa vile Serikali ya Mapinduzi  ya Zanzibar iko katika mpango wa  kumaliza kabisa maradhi ya malaria Nchini ambayo hivi sasa yamepunguwa kwa hatua kubwa sana “. Alieleza Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Uturuki kupitia Taasisi zake za Misaada ya maendeleo ya vyuo Vikuu kwa jitihada zake inazochukuwa za kusaidia huduma za kijamii kwa mataifa rafiki ikiwemo Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
“ Wapo wataalamu wetu wengi wa fani ya afya waliowahi kupata mafunzo yao ya juu nchini Uturuki  hatua ambayo kwa kiasi kikubwa inaendelea kuipunguzia mzigo  kubwa Serikali  kwa kumsafirisha mgonjwa nje ya Zanzibar kwa matibabu ambao wengi kati yao hivi sasa wanayapata hapa hapa Nchini “. Alifafanua Balozi Seif.
Naye Kiongozi wa Madaktari hao kutoka  Chuo Kikuu cha Fatih kinachoshughulikia masuala ya matibabu na utafiti kutoka Jamuhuri ya Uturuki  Profesa Mkuu wa Upasuaji  Omer Faruk Akinci alisema tatizo kubwa la Jamii linaloleta fadhaa na hatimae kutumbuka kwa maradhi tofauti ni msongamano wa mawazo yasiyokwisha.
Profesa Omer Faruk alisema kitu pekee kitakachoisaidia  jamii popote pale katika kupunguza wimbi hilo la mawazo ni kwa wana jamii wenyewe kuelekeza nguvu zao zaidi katika kujipatia  taaluma ambayo ndio mkombozi wa yote.
Wakitoa salamu katika kikao hicho wadhamini wa Madaktari hao wa Uturuki  Profesa Seif Ali Tekalan kutoka Chuo Kikuu cha Fatih na Profesa MuratTuncer wa Chuo Kikuu cha Hacettepe Nchini humo walisema vyuo vyao hivi sasa vina jumla ya wafanuzi 25 wanaosomea fani  tofauti  kutoka Tanzania   Bara pamoja na Zanzibar.
Walisema wakati Taasisi zao zimejikita zaidi katika kuimarisha sekta ya elimu kuanzia skuli hadi vyuo vikuu zimelenga  kuongeza zaidi idadi ya viwango vya wanafunzi  wanaotoka Tanzania.
Wametoa mwaliko kwa wanafunzi wa Tanzania kushiriki katika mashindano yatakayoandaliwa na vyuo vikuu hivyo hapo baadae katika masuala ya elimu yakijikita zaidi  kwenyea masuala  ya Utamaduni.
Mapema Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Juma Duni Haji alisema ushirikiano uliopo kati ya wananchi wa Mataifa ya Jamuhuri ya Uturuki na Zanzibar ni dalili nzuri ya uhusiano mwema kati ya pande hizo mbili.
Waziri Juma Duni Haji alishauri dalili hiyo nzuri ya uhusiano inapaswa kuendelea kuenziwa na kuimarishwa kwa ustawi wa vizazi vijavyo vya pande zote mbili rafiki.
Madaktari hao  wa Jamuhuri ya Uturuki  walipata fursa ya kutoa huduma mbali mbali za afya katika hospitali za Mnazi Mmoja, Nungwi, Kitope, Kivunge, Makunduchi kwa unguja na  Chake chake wete, Mkoani na Vitongoji kwa Pemba.
Serikali ya Jamuhuri ya Uturuki kupitia Taasisi zake za vyuo vikuu vya mambo ya Afya imekuwa ikitoa msaada wa kiafya kwa kuwashirikisha madaktari wake wanaojitolea kuja kufanya kazi hapa Zanzibar kwenye mpango wake maalum ulioasisiwa tokea mwaka 2007.


Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
2/9/2013.





Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania { JWTZ } Meja Khatibu Shaaban Mshindo aliyefariki Dunia akiwa katika shughuli za ulinzi wa amani katika kikosi  cha umoja wa Mataifa kwenye jimbo la Goma Nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo amezikwa kwa heshima zote za Kijeshi.
Meja Shaaban ambaye alijeruhiwa vibaya kwa bomu katika eneo lake la kazi na kusababisha kuvuja damu nyingi na hatimae kusababisha kifo chake akiwa njiani kupelekwa Hospitali alizikwa kijiji kwao Mangapwani Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa Kaskazini Unguja.
Makamanda na wapiganaji wa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania , askari wengine wa vikosi vya ulinzi, wananchi , ndugu wa marehemu walishiriki kwenye mazishi hayo wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohammed Aboud Mohammed.
Marehemu Meja Khatib Shaaban Mshindo alizaliwa Tarehe 29 Septemba 1972 katika Mtaa wa Rahaleo Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi na baadaye kupata elimu yake ya msingi na kuhitimu mwaka 1986.
Alijiunga na Skuli ya Sekondari uchama na kuhitimu kidato cha Nne mwaka 1990 ambapo baadaye akajiunga na kidato cha tano na sita katika skuli ya sekondari ya Alharamain na kumaliza mwaka 1993.
Meja Khatib Shaaban Mshindo alijiunga na Jeshi la wananchi wa Tanzania             { JWTZ } Tarehe 1 machi 1995 na kutunukiwa heshima ya kamisheni tarehe 17 mei 1997.
Katika utumishi wake Meja Khatib Shaaban Mshindo alibahatika kuhudhuria mafunzo ya afisa mwanafunzi chuoni Monduli, kozi ya uongozi wa platuni, uongozi wa kombania pamoja na mafunzo ya operesheni Nchini Canada mwaka 2008.
Kamanda Khatib kutokana na ukakamavu wake alipandishwa vyeo kuanzia nafasi ya Luteni mwaka 1998, kepteni mwaka 2004 na kufikia cheo cha meja mwaka 2010 wadhifa aliokuwa nao hadi kufariki kwake.
Marehemu Meja Khatibu Shaaban Mshindo aliwahi kushika madaraka ya Kamanda wa Kikosi mwaka 1997, Mkufunzi kuanzia mwaka 2000  hadi mwaka 2006 pamoja na kuwa kamanda wa kombania Mkoani Kibaha.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua na kuthamini mchango wa Meja Khatibu Shaaban Mshindo alimtunuku nishani ya Miaka 40 ya JWTZ.
Umoja wa Mataifa katika mazishi hayo uliwakilishwa na Kamanda wa Vikosi vya Umoja huo Mjini Goma Nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Meja D.B Samujeli .
Kamanda Khatibu Shaaban Mshindo aliyelitumikia jeshi la Wananchi wa Tanzania katika kipindi cha miaka 18 miezi saba na siku 28 ameacha kizuka mmoja na watoto watatu.
Mwenyezi Muungu alilaze roho ya marehemu Meja Khatibu Shaaban Mshindo mahali peMa peponi. Amin.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
1/9/2013.

Sunday, 25 August 2013

Rais Dk.Shein afanya mabadiliko ya Wizara mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha  Salum Maulid Salum, kuwa Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora,katika hafla iliyofanyika Ukumbi
wa Ikulu Mjini Zanzibar.[Picha na Ramadhan
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha Joseph Abdalla Meza,kuwa Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ,katika hafla
iliyofanyika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha Mwinyiussi A.Hassan,kuwa Naibu Katibu
Mkuu (Tawala za Mikoa)  katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa ikulu
Mjini Zanzibar
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha CDR Julius Nalimy Maziku,kuwa  Naibu
Katibu Mkuu (Idara Maalum za SMZ) katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa
ikulu Mjini Zanzibar
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha  Yakout Hassan Yakout, kuwa  Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma,katika hafla
iliyofanyika Ukumbi wa ikulu Mjini Zanzibar
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akimuapisha ALI Khamis Juma,kuwa Naibu Katibu
Mkuu (Ustawi wa Jamii Vijana Wanawake na Watoto),katika hafla
iliyofanyika Ukumbi wa ikulu Mjini Zanzibar























Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Naibu
katibu Wakuu wa Wizara mbali mbali baada ya kuwaapisha Ikulu Mjini
Zanzibar leo jioni.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Viongozi wa CCM wakati wa hafla ya Kulizindua rasmi Baraza la ushauri la Viongozi wakuu wa CCM Makao Makuu Mjini Dodoma.

 Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Viongozi wa CCM wakati wa hafla ya Kulizindua rasmi Baraza la ushauri la Viongozi wakuu wa CCM Makao Makuu Mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dr. Jakaya Mrisho Kiwete akibonyeza kitufe kuashiria kulizindua Baraza la ushauri la Viongozi wakuu wa CCM Makao Makuu Mjini Dodoma.

 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dr. Jakaya Mrisho Kiwete akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la ushauri la Viongozi wakuu wa CCM mara baada ya kulizindua  rasmi Makao Makuu Mjini Dodoma.Kulia yake ni Mzee Ali Hassan mwinyi, Mzee John Malecela,Rais wa Zanzibar Dr. AIi  Mohammed Sheni  na Mh. Mizengo Pinda. Na Kushoto ya Dr. Kiwete ni Mh. Benjamin Mkapa, Dr. Amani Abeid Karume na Mh. Pius Msekwa.

 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dr. Jakaya Mrisho Kiwete akiingia katika viwanja  vya Makao Makuu wa Chama hicho Mjini Dodoma akiwa ni viongozi wa Baraza la ushauri la Viongozi wakuu wa CCM alilolizindua rasmi.

 Mwenyekiti Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi Mh. Benjamin William Mkapa akibadilishana mawazo na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Amani Abeid Karume katika hafla ya uzinduzi ya Baraza la Ushauri la Viongozi  wakuu wa CCM Mjini Dodoma.
























Mwenyekiti mstaafu wa CCM Mzee Ali Hassan Mwinyi akizungumza na Makamu mwenyekiti wa CCM na Rais nwa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Sheni katika hafla ya uzinduzi ya Baraza la Ushauri la Viongozi  wakuu wa CCM Mjini Dodoma.

Press Release:-
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinzuzi Taifa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alisema kuundwa kwa Baraza la ushauri la Viongozi Wakuu wa Chama Cha Mapinduzi ni  fursa maalum na nzito itakayosaidia kuimarisha zaidi nguvu ya Chama hicho.
Dr. Kikwete alisema hayo katika hafla maalum ya uzinduzi wa Baraza hilo linalojumuisha Wenyeviti, Makamu wenyeviti na Makatibu wakuu wastaafu wa Chama hicho iliyofanyika katika viwanja vya Makamu Makuu ya Chama hicho yaliyopo katika Manispaa ya Dodoma.
Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa alifahamisha kwamba Wajumbe wa Baraza hilo watakuwa na uwezo kamili wa kushauri hata kuingia katika Vikao vya Juu vya CCM katika masuala mazito yatakayokijengea mustakabala mzuri wa baadae chama hicho.
Dr. Kikwete alieleza kuwa Uongozi wa CCM ulifikia uwamuzi wa kuundwa kwa Baraza hilo katika Mkutano wake Maalum wa nane Novemba Mwaka 2012 kupitia Ibara ya 127 ya chama hicho baada ya kutambua na kuheshimu mchango wa Viongozi hao.
Alisema Wana CCM  wanastahiki kujipongeza kutokana na ushauri huo ambao uliwahi kupingwa wakati wa nyuma kwa hofu ya Kikundi hicho kutengeneza fitina za kumuingilia Rais katika maamuzi mazito.
Dr. Kikwete alisema Tanzania imepata mafanikio makubwa kutokana na mabadiliko ya Kiuchumi na hata utulivu wa kisiasa kufuatia mchango wa Viongozi wastaafu ambao kwa sasa watakuwa wakitoa mawazo yao kwa chama kupitia Baraza hilo.
Dr. Kikwete alimtolea mfano  Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mzee Ali Hassan Mwinyi kuwa ni wa kwanza wa mabadiliko ya Uchumi na Siasa ndani ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika miaka ya mwishoni mwa 80 na mwanzoni mwa 90.
“ Mzee Mwinyi ametuongoza katika mabadiliko  hayo ya kiuchumi sambamba nay ale ya mfumo wa vyama vingi vya kisiasa NchinibnTanzania licha ya yeye kutowahi kuufanyika kazi Mfumo huo “. Alifafanua Dr. Kiwete.
“ Ukweli tuseme mageuzi ya kiuchumi yaliyofanyika Tanzania chini ya uongozi wa Mzee Mwinyi wengine wakimwita Mzee Ruksa mimi ndie  niliyeanza kuyafaidi katika kazi zangu za Urais “. Alisisitiza Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.
Aliongeza kwamba mfumo huo wa kuundwa kwa Baraza la Ushauri la Viongozi wa Wakuu wa Chama Cha Mapinduzi litaondoa usumbufu wa kuwapa tabu wazee hao wa kuitwa mara kwa mara katika Vikao vya Chama kwa lengo la kupata ufumbuzi wa mambo.
Alisema kwa mujibu wa kanuni za CCM Ibara ya 127 Baraza hilo litakuwa na uwezo kamili wa kushauri hata ndani ya Vikao vya juu vya Chama ama kwa kushiriki wajumbe wote wa baraza au hata uwakilishi wao.
Mapema Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdullrahman Kinana alisema Baraza hilo linalojumuisha Marais wastaafu wa Serikali ya Muungano na Wenyeviti wastaafu wa CCM Taifa Marais wastaafu wa Zanzibar kupitia  na Makamu Wenyeviti wastaafu CCM Zanzibar na Bara litafanya vikao vyake kwa mujibu wa utaratibu watakaojipangia wenyewe.
Katibu Mkuu wa CCM Kikana alisema wajumbe wa Baraza hilo watakuwa na fursa ya kutoa ushauri kwa Serikali zinazoongozwa na Chama cha Mapinduzi Bara na Zanzibar.
Viongozi hao wanaounda Baraza hilo la Ushauri la Viongozi wakuu wa CCM waliopata fursa ya kuhudhuria uzinduzi huo ni pamoja na Mwenyekiti mstaafu wa CCM na Rais Mstaafu wa SMT awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na aliyemfuatia Mh. Benjamin William Mkapa.
Wengine waliohudhuria ni Makamu mwenyekiti Msaafu na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dr. Amani Abeid Karume pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mh. Pius Msekwa.
Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dr. Salimin Amour hakuhudhuria hafla hiyo kutokana na sababu za kiafya wakati Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Phillip Mangula yeye alikuwa na udhuru wa msiba.
Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alibonyeza kitufe maalum kuashiria kuzindua  Baraza hilo hafla iliyoambatana na ngoma za vikundi vya utamaduni pamoja na muziki wa kizazi kipya.
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
24/8/2013.
 

Wednesday, 21 August 2013

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika ziara ya kuzitembelea Taasisi za SMZ zilizopo Dar.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Bima Zanzibar aliyepo kulia yake Dr. Hamed Rashid Hikman, ambapo  kushoto yake ni Mkuruigenzi Mtendaji wa Shirika hilo Abdulnaasir Abdulrahman kabla ya kuzungumza na watendaji wa shirika hilo tawi la Lumbumba Jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na watendaji wa shirika la Bima Zanzibar Tawi la Lumbumba Jiijini Dar es salaa alipofanya ziara ya kuzitembelea Taasisi za SMZ zilizopo Dar.

 Meneja wa Benki ya watu wa Zanzibar { PBZ } Tawi la Kariakoo Jijijni Dar es salaam Badru Idd akitoa maelezo ya utendaji wa tawi hilo na Lile ya Benki ya Kiislamu liliopo Lumumba mbele ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyekuwa katika ziara maalum ya kutembelea Taasisi za SMZ zilizopo Jijini Dar.
Pembeni yao kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Makao Makuu Zanzibar Juma Amour Mohammed.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na watendaji wa shirika la Bima Zanzibar Tawi la Lumbumba Jiijini Dar es salaa alipofanya ziara ya kuzitembelea Taasisi za SMZ zilizopo Dar.























Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na watendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar wa Matawi ya Kariakoo na Lumbumba kwenye ukumbi wa Tawi la Benki hiyo inayotoa huduma za Kiislamu uliopo Lumumba Jijini Dar es salaam.
Picha na Hassan Issa wa –OMPR – ZNZ.
Press Release:-
Jitihada kubwa zinazoendelea kuchukuliwa na Uongozi pamoja na Wafanyakazi wa Shirika ya Bima la Zanzibar { ZIC } na ule wa Benki ya Watu wa Zanzibar          { PBZ } ndizo zilizopelekea  kuongezeka zaidi kwa idadi ya wananchi na wateja wanaohitaji kupata huduma katika Taasisi hizo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo mara baada ya kuzitembelea ofisi za Taasisi hizo zinazotoa huduma katika Jiji la Dar es salaam na kuelezea kuridhika kwake na utendaji bora wa kisasa uliofikiwa na mashirika hayo.
Balozi Seif alisema  licha ya kuvutiwa sana na utaratibu wao wa makusanyo ya mapato na matumizi ya wastani lakini bado watendaji wa taasisi hizo wanapaswa kujituma zaidi katika mbinu za kutafuta wateja kwa lengo la kwenda sambamba na ushindani uliopo wa kibiashara.
Alifahamisha kwamba mbinu za kumchunga mteja wakati wote zitafanikiwa endapo juhudi za ziada za utoaji huduma kwa mwendo wa kasi kupitia watendaji hao zitachukuliwa.
“ Tuna kila sababu ya kuyapongeza mashirika yetu haya kutokana na huduma zao zinazokwenda kwa kasi. Haya ni miongoni mwa mashirika yanayoinawisha uso Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Tuna haki ya kujivunia “. Alifafanua Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliziagiza Taasisi hizo za Bima na PBZ mbali ya kuendelea kujitangaza lakini pia kufikiria kuongeza matawi mengine zaidi katika maeneo yenye mkusanyiko wa wananchi wengi yakiwemo yale ya Vijijini ili huduma zao ziwe za uwiano katika maeneo yote ya hapa Nchini.
Alieleza katika kuzipa nguvu zaidi taasisi hizo Serikali Kuu itaangalia utaratibu wa kuzikatia Bima mali zake yakiwemo majengo mapya ya Ofisi za Serikali zinazoendelea kujengwa katika maeneo tofauti Nchini.
“ Hata nyumba zangu niko tayari kuzikatia bima, kinachohitajika kwa sasa ni nyinyi watendaji kunishawishi hadi nifikie kiwango cha kutekeleza wazo hilo muhimu “. Alieleza Balozi Seif.
“ Tumekuwa pia tukishuhudia mikopo mikubwa inayotolewa na Benki ya Watu wa Zanzibar na  ii ni vyema ikaenda samba mba na uwekaji wa bima ya maisha ili kunusuru kiwango kikubwa cha mikopo kinachotolewa endapo mkopaji mwenyezi Muungu atamuhitaji “. Aliendelea kufafanua Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Akitoa Taarifa ya Shirika la Bima Zanzibar na Utekelezaji wake  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Abdulnaasir Abdulrahman alisema hali ya soko inaendelea kuwa ya ushindani ambapo biashara kubwa ikitawaliwa na ile ya kinga za magari.
Alisema biashara hiyo inachangia zaidi ya asilimia 80% ya biashara yote hali inayopelekea uongozi wa shirika kufanya juhudi za kuandikisha biashara nyengine ambazo zina faida kubwa ikilinganisha na ya magari.
Mkurugenzi huyo wa shirika la Bima alifahamisha kwamba shirika hilo limeweza kukusanya zaidi ya shilingi Bilioni 1.1 kutoka katika vianzio vyake mbali mbali sawa na asilimia 86% ya lengo lake ambalo ni kukusanya shilingi Bilioni 12.3 kwa mwaka 2013.
Abdulnaasir alisema Kanda ya Pwani Dar es salaam ni tegemeo kubwa la shirika kwa makusanyo yake ambapo katika kipindi cha  Januari hadi Juni mwaka huu Ofisi hiyo tayari imeshakusanya shilingi Bilioni 2.1 ikiwa ni sawa na asilimia 87% ya makadirio ya mwaka.
Alisema katika kukabiliana na ushindani wa kibiashara shirika lake licha ya kufanya kazi zake Zanzibar lakini pia  limeweza kujitanua kwa kufungua ofisi zaidi katika kanda za Pwani- Dar es salaam, Arusha, Mwanza, mbeya, Dodoma na Mtwara.
Naye akitoa Taarifa ya maendeleo ya Matawi ya Benki ya Watu wa Zanzibar yaliyopo Kariakoo na Lumumba Mjini  Dar es salaam Meneja wa Tawi la Kariakoo Badru Idd  alisema PBZ ilipanga kuwafuata wateja wake waliopo na wanaokwenda Tanzania Bara kikazi, kibiashara, kimasomo na wanaopita ambao wanahitaji huduma za Kibenki.
Meneja Badru alisema pamoja na kuwepo kwa ushindani mkubwa wa kibiashara lakini matawi hayo yameweza kufungua hesabu za wateja mbali mbali na kufikia elfu 8,360 kutoka 3,209 ikiwa ni ongezeko la asilimia 160% .
Alifahamisha kwamba amana za wateja zimekuwa kwa kiwango kizuri na kufikia Shilingi Bilioni 24.58  mwezi agosti mwaka 2013 wakati disemba 31 mwaka 2011 zilikuwa Shilingi Bilioni 3.99 ikiwa ni ongezeko la asilimi 516%.
Baadae Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alikutana na Uongozi wa shirika la Meli na Uwakala Zanzibar Tawi la Dar es salaam na kuwaasa kwamba wana kazi kubwa ya kulihudumia shirika hilo katika mazingira ya uwajibikaji.
Balozi Seif alisema shirika hilo linaweza kupoteza imani ya wateja kwa kufikia hatua ya kukata tamaa endapo uendeshaji wa taasisi hiyo hautakuwa wa kiwango na uhakika.
Shirika la Meli na uwakala limeasisiwa mwaka 1978 likiwa na Meli sita zikiwemo mbili zilizorithiwa kutoka ukoloni ambazo zilikuwa zikitoa huduma katika mwambao wa Afrika ya mashariki kuanzia Mtwara Tanzania, Zanzibar, Tanga hadi Mombasa Nchini Kenya.
Mapema mchana Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alifanya mazungumzo na Uongozi wa Shirika la Taifa la Biashara Zanzibar { ZSTC } ambapo aliushauri uongozi wa shirika hilo kuanzisha utaratibu wa kuwasaidia wafanyabiashara wadogo wadogo kwa kuwapatia bidhaa zinazozalishwa Tanzania Bara kwa bei nafuu.
Balozi Seif alisema utaratibu huo unaweza kutoa fursa zaidi ya kuongeza kipato cha wafanyabiashara hao ambao wengi hawana uwezo wa kufuatilia bidhaa hizo katika maeneo mbali mbali ya mIkoa ya Tanzania Bara.
Akitoa Taarifa fupi Naibu Mkurugenzi muendeshaji wa shirika la Taifa la Biashara Zanzibar { ZSTC } Suleiman Juma Jongo alisema lisha ya shirika hilo lililoasisiwa katika miaka ya 70 kuendesha shughuli za ununuzi na uuzaji wa karafuu lakini bado lina fursa ya  kuendelea kuwepo kutokana na umuhimu wake kiuchumi.
 
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
22/8/2013.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika ziara yake katika Taasisi za SMZ zilizopo Mjini Dar es salaam.

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa na Mkurugenzi wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dar es salaam Shumbana Taufiq kabla ya kuanza ziara yake katika Taasisi za SMZ zilizopo Mjini Dar es salaam.
 Kulia yao ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Issa Mlingoti.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akisaini kitabu cha wageni mara alipowasili katika jengo la Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar liliopo Mjini Dar es salaam akikaribishwa na Mkurugenzi wa Ofisi hiyo  Shumbana Taifiq.

 Balozi Seif akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha ZBC Dar Msangu Said Mohammed alipotembelea chumbna cha Habari cha Kitengo hicho.
Kulia yake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Issa Mlingoti na Kushoto yake ni Mkurugenzi Mkuu wa ZBC Hassan Mitawi.
 





















Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Zanzibar Juma Ameir akimuelezea Balozi Seif namna Wizara hiyo inavyojaribu kutatua baadhi ya changa moto wanazopambana nazo  watendaji wa Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za Serikali waliopo Dar es salaam.

Press Release:-
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itajitahidi kuona changamoto zinazowakabili watendaji wa Ofisi ya Uratibu wa shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar waliopo Dar es salaam zinashughulikiwa vyema kwa kupatiwa ufumbuzi ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofanya ziara maalum ya kuangalia shughuli za kazi za watendaji wa Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizopo Dar es salaam akianzia na Ofisi ya Uratibu wa shughuli za Serikali.
Ofisi hiyo  iliyopewa mamlaka ya kuratibu uwajibikaji wa Taasisi zote za SMZ zilizopo Mjini Dar es salaam  itakuwa  chini ya Ofisi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Sheni katika baadhi ya Taasisi za Serikali siku moja iliyopita.
Balozi Seif alisema  Serikali iliamua kwa makusudi kuanzisha Ofisi hiyo mnamo mwaka 1986 kwa lengo la kuwa kiunganishi cha upatikanaji wa huduma za kiuchumi kiurahisi kati ya Zanzibar na Tanzania Bara sambamba na mashirika pamoja na Taasisi za Kimataifa.
Katika  mbinu za kujaribu  kupunguza  matumizi  ya uendeshaji wa Ofisi Balozi Seif alifahamisha kwamba Serikali ina nia ya kulipata jengo hilo kwa kuwasiliana na Serikali ya Muungano hata kwa njia ya kubadilishana { Butter system } jambo ambalo gharama zinazotumika hivi sasa zinaweza kusaidia masuala mengine.
Akizungumzia Kitengo cha Habari kilichojumuisha Magazeti ya Serika { Zanzibar Leo }, shirika la Utangazaji Zanzibar { ZBC } na Habari Maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwapongeza wana Habari hao kwa umahiri wao wa kufanya kazi licha ya kuzunguukwa na mazingira magumu ya kikazi likiwemo tatizo la usafiri .
Aliuagiza Uongozi wa Taasisi hizo kufanya utaratibu wa kuandika mapendekezo  ya vile vifaa muhimu zaidi  vya mwanzo na kuyawasilisha Serikalini ili kuangalia namna ya kusaidia uwezeshaji.
Balozi Seif alisema kutokana na mabadiliko ya haraka na ya kila wakati katika sekta ya Habari, watendaji wake wanalazimika nao muda wote waende na wakati.
“ Kwa vile Serikali Kuu tumeshaamua Sekta zetu za Habari zijiendeshe kibiashara. Sasa Baraza letu la Wawakilishi kuanzia mwezi Oktoba katika vikao vijavyo litalazimika kulipa matangazo ya moja kwa moja ya vituo vya Habari vya  ZBC Redio na Tv “. Alisisitiza Balozi Seif.
Aliuagiza Uongozi wa Sekta ya Habari kufanya utafiti utakaofahamu tatizo linalosababisha matangazo ya ZBC Redio na Televisheni kutopatikana katika maeneo ya Tanzania Bara.
“Mimi nilikuwa msikilizaji mkubwa wa Vipindi vya Redio hasa kile cha kutoka magazetini hakinipiti ninapokuwa Dar pamoja na matangazo ya ZBC TV. Hata nikiwa Dodoma Matangazo ya Redio nilikuwa nikiyapa lakini sasa yote yamekatika siju kwa nini? “ Aliuliza Balozi Seif.
Mapema Mkurugenzi wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dar es salaam Shumbana Taufiq alisema Taasisi hiyo ambayo ni kiunganishi muhimu cha mawasiliano kati ya Zanzibar na Mashirika na Taasisi za Kimataifa imekuwa na mazingira magumu ya utekelezaji wa majukumu yake kutokana na tatizo la kutoingiziwa fedha kwa wakati.
Mkurugenzi Shumbana alisema gharama za kupanda kwa maisha hasa katika Jiji la Dar es salaam kumewafanya watendaji hao kuishi katika maisha ya kubahatisha suala ambalo hupunguza ari na moyo wa uwajibikaji.
“ Wakati mwengine sisi wasimamizi tunakuwa katika hali ya unyonge wakati hata zile fedha za pencheni kwa wafanyakazi wastaafu zinachelewakutufikia na matokeo yake kuleta malalamiko kwa wazee wetu hao waliopo hapa Dar “. Alifafanua Mkurugenzi Shumbana.
Nao baadhi ya watendaji wa taasisi hizo wakiwemo viongozi wao wa Wizara na Idara wamezitaja baadhi ya changa moto zinazokwaza utekelezaji wao wa kazi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya kazi, usafiri pamoja na kuomba kuongezewa posho ili kukidhi mahitaji.
Awali  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alizitembelea Ofisi ya Idara ya Uratibu, Kitengo cha Utawala na Rasilmali Watu, uratibu wa misaada na Mipango pamoja na ile ya wana Habari.
 
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
21/8/2013.