Friday, 6 June 2014

balozi Seif Aipongeza Timu ya Ujamaa kwa Kupanda Daraja.




 Rais wa Klabu ya Ujamaa ya Rahaleo Othman Mussa akielezea mikakati ya Timu yake kushiriki mashindano ya 12 bora daraja la Pili Unguja mbele ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.kushoto ya Othman Mussa ni mwenyekiti wa Klabu ya Ujamaa Ameir Makungu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiipongeza timu ya soka ya Ujamaa baada ya kupanda daraja ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini.
 Balozi Seif akiwa na Kombe la Ubingwa Daraja la Pili Wilaya ya Mjini, akifurahia baada ya kukabidhiwa Ofisini kwake na Uongozi wa timu ya Ujamaa baada ya kulitowa Kombe hilo la Ubingwa lililonyakuliwa na wakongwe wa Soka Unguja Timu ya Ujamaa daraja la pili Wilaya ya Mjini.wa mwanzo kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar { BTMZ } Sharifa Khamis na Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi akiwa pia muasisi wa Timu pinzani dhidi ya Ujamaa Timu ya Muembeladu { Kubwa Lijalo } Mh. Abdulla Mwinyi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiipongeza timu ya soka ya Ujamaa baada ya kupanda daraja ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini.
Balozi Seif, akisalimiana na Viongozi wa Timu ya Ujama walipofika Ofisini kwake kumkabidhi Kombe la Ubingwa wa Wilaya ya Mjini kwa kuwa Mabingwa wa Ligi Hiyo kwa Mwaka 2014.

Timu Kongwe ya Mchezo wa Soka hapa Zanzibar Ujamaa Sports Club imejizatiti kurejea tena kwenye ligi kuu ya Zanzibar Daraja la Kwanza baada ya kuteremka kiwango chake na kufikia hadi Daraja la Tatu mwaka 2013.

Rais wa Klabu ya Ujamaa yenye mastakimu yake Mtaa wa Rahaleo Mkabala na Shirika la Utangazaji Zanzibar { ZBC – Redio } Othman Mussa alieleza hayo Wakati Uongozi pamoja na baadhi ya wachezaji wa Timu hiyo ulipofika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kumsalimia baada ya kutawadhwa rasmi kuwa mabingwa wa Soka Daraja la Pili Wilaya ya Mjini.

Othman Mussa  alimueleza Balozi Seif ambae pia ni Mchezaji wa Zamani wa Klabu hiyo kwamba ipo dalili kubwa kwa timu hiyo kongwe kupanda daraja na kufikia malengo kutokana na ari na mashirikiano makubwa yaliyopo kati ya wachezaji na Viongozi wa Klabu hiyo.

Hata hivyo Rais huyo wa Klabu ya Ujamaa alieleza kwamba zipo baadhi ya changa moto zinazoikabili timu hiyo kwa hivi sasa ikiwa ni pamoja na gharama za huduma kwa vile wako katika maandalizi ya kujenga kambi kwa ajili ya kukabiliana na fainali ya mashindano ya  timu 12 Bora za soka Wilaya za Unguja.

Naye Katibu Mkuu wa Klabu ya Ujamaa Juma Khalfan alieleza kwamba Timu hiyo ilifikia hatua ya ubingwa baada kazi kubwa ya mashindano ya ligi ya soka ya Daraja la Tatu iliyozikutanisha takriban Timu 22 zilizomo ndani ya Wilaya ya Mjini.

Juma Khalfan alifahamisha kwamba klabu ya Ujamaa ambayo ina historia ndefu ya mchezo wa soka  hapa Nchini iliwahi kuchukuwa ubingwa wa Zanzibar wa mchezo huo katika miaka ya nyuma.

Akitoa shukrani zake kufuatia ubingwa huo walioupata Klabu ya Ujamaa wa Soka Wilaya ya Mjini Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Uongozi na Wachezaji wa Timu hiyo bado wana kazi kubwa ya kuhakikisha hadhi ya timu hiyo kisoka inarejea tena.

Balozi Seif alisema aliwasisitiza wachezaji wa timu hiyo kudumisha nidhamu wakati wanapokuwa michezoni kwa kutii uamuzi wa wachezeshaji soka ili lengo la kuimarisha uanamichezo lifanikiwe vyema.

“ Itapendeza na kufurahisha iwapo itafikia wakati timu yetu inatoa wachezaji wa Kitaifa na Kimataifa. Kwa nini wachezaji wetu wasifikie kiwango cha akina drogba, Eto, Song na wengineo wanaotoka ndani ya Bara la Afrika ? “. Aliuliza Balozi Seif.

Alisema kwa vile wachezaji wa Timu hiyo wameshaamua kuweka kambi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano ya 12 bora Daraja la Pili Kanda ya Unguja ataangalia uwezekano wa kuongeza nguvu zake ili wafikie lengo walilojiwekea.

Monday, 17 March 2014

Ripoti ya ajali ya Mv Kilimanjaro II

Mwenyekiti wa Bodi ya kuchunguza ajali ya Meli ya MV. Kilimanjaro II Khamis Ramadhan Abdallah (kushoto) akikabidhi Ripoti ya Bodi hiyo baada ya kukamilika kwa Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano Rashid Seif Suleiman Ofisini kwake Kisauni nje kidogo ya mji wa Zanzibar
Mwenyekiti wa Bodi ya kuchunguza ajali ya Meli ya MV. Kilimanjaro II Khamis Ramadhan Abdallah (kushoto) akikabidhi Ripoti ya Bodi hiyo baada ya kukamilika kwa Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano Rashid Seif Suleiman Ofisini kwake Kisauni nje kidogo ya mji wa Zanzibar
   
Bodi ya kuchunguza ajali ya Meli ya MV. Kilimanjaro II leo imekabidhi rasmi Ripoti ya ajali hiyo baada ya kumaliza kazi hiyo kwa Waziri wa  Miundo mbinu na Mawasiliano Rashid Seif Suleiman Ofisini kwake Kisauni nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Akikabidhi Ripoti hiyo Mwenyekiti wa Bodi hiyo Khamis Ramadhan Abdallah amesema kazi hiyo waliyopewa wameweza kuimaliza kwa mujibu wa siku walizopewa na walikuwa huru bila ya kuingiliwa na mkono wa Serikali wala Taasisi yoyote.
Aidha alisema Bodi ilifanya kazi katika mazingira magumu lakini walichukulia kazi hiyo niyanyumbani na niwajibu wao kufanya kwa Maslahi ya wananchi wa Zanzibar.
Hata hivyo alisema hapo awali kazi hiyo walipangiwa kuifanya kwa kipindi cha mwezi mmoja lakini kutokana na uzito wa kazi hiyo na majukumu mengine walilazimika kuomba mwezi mmoja ambapo kazi hiyo walitakiwa kuikabidhi kesho na badala yake wameweza kuikabidhi leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya kuchunguza ajali ya Meli ya MV. Kilimanjaro II, Khamis Ramadhan Abdallah (katikati) akisoma baadhi ya vipengele vya Ripoti hiyo wakati wa kumkabidhi  Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano Zanzibar Rashid Seif Suleiman (mwenye kanzu) Ofisini kwake Kisauni nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Picha - Nafisa M. Ali
Mwenyekiti wa Bodi ya kuchunguza ajali ya Meli ya MV. Kilimanjaro II, Khamis Ramadhan Abdallah (katikati) akisoma baadhi ya vipengele vya Ripoti hiyo wakati wa kumkabidhi Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano Zanzibar Rashid Seif Suleiman (mwenye kanzu) Ofisini kwake Kisauni nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Picha – Nafisa M. Ali
Aidha Mwenyekiti huyo alitoa shukran zake za dhati kwa niaba ya bodi hiyo kwa mamlaka ya Usafiri Baharini kwa ushirikiano mzuri waliouonesha kwa bodi hiyo kwa kipindi chote cha kazi hiyo.
Kwa upande wake Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Rashid Seif Suleiman ameipongeza Bodi hiyo kwa kufanya kazi bila ya upendeleo na zaidi walizingatia uhalisia wa kazi yao na siyo kubabaishwa na Mtu.
Aidha alisema chombo hicho hakikuundwa kwa kutafutwa nani mbaya wala mkosa wa ajali hiyo bali kimeundwa kwa ajili ya kuangalia mapungufu yaliyopo na kuweza kurekebishwa ili Wazanzibari wasizidi kuumia.
Hata hivyo alisema dalili nzuri ipo katika Ripoti hiyo na kazi iliyobaki ni kuisoma kwa kina na kisha kukabidhi katika Mikono ya Serikali kuu kwa mujibu wa taratibu zilizopo.
Aidha aliishukuru sana bodi hiyo kwa vile ilikuwa huru na kuweza kufanya kazi kwa kina bila kizuizi cha mtu wala Serikali.
Naye Naibu Katibu mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Tahir A.K Abdullah amesema Wananchi hivi sasa wanasubiri kuona Serikali imefanya nini tokea ajali hiyo imetokea ambapo aliwatoa wasiwasi kuwa haki  itatendeka kwa mujibu wa uchunguzi uliofanyika.
Bodi hiyo ya Wajumbe watano ambayo iliyoundwa chini ya Sheria ya Usafiri wa Baharini kifungu no. 4552 na 4551 ya mwaka 2006 imeundwa kufuatia ajali ya Meli ya MV.
Kilimanjaro II iliyotokea miezi miwili iliyopita katika mkondo wa Nungwi ilipokuwa ikitokea Pemba kuja Unguja.

Mkutano wa Wawekezaji wa Israel na Tanzania

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua mkutano wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kati ya Israel na Tanzania, katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua mkutano wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kati ya Israel na Tanzania, katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipongezwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene, baada ya kufungua rasmi mkutano wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kati ya Israel na Tanzania, katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Regnald Mengi (wa pili kulia) ni Mwakilishi wa Ubalozi wa Israel kwa nchi za Tanzania, Kenya Uganda na Seychells, Gilad Millo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipongezwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene, baada ya kufungua rasmi mkutano wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kati ya Israel na Tanzania, katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Regnald Mengi (wa pili kulia) ni Mwakilishi wa Ubalozi wa Israel kwa nchi za Tanzania, Kenya Uganda na Seychells, Gilad Millo
Baadhi ya washiriki wa mkutano wakimsikiliza  Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akiwahutubia
Baadhi ya washiriki wa mkutano wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akiwahutubia
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mkutano
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mkutano. Picha – OMR
About these ads

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwapa pole baadhi ya Wananchi ambao nyumba zao zilikumbwa na upepo mkali katika Shehia za Kwaalamsha, Makadara na Mkele Wilaya ya Mjini

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwapa pole baadhi ya Wananchi ambao nyumba zao zilikumbwa na upepo mkali katika Shehia za Kwaalamsha, Makadara na Mkele Wilaya ya Mjini
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwapa pole baadhi ya Wananchi ambao nyumba zao zilikumbwa na upepo mkali katika Shehia za Kwaalamsha, Makadara na Mkele Wilaya ya Mjini
Jamii Nchini imetahadharishwa kuwa makini katika kipindi hichi kilichoanza cha msimu wa mvua za masika ambacho kimezoeleka kuwa na matukio mbali mbali ya maafa yanayoleta athari kwa wananachi.
Tahadhari hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akiwafariji wananchi waliokumbwa na maafa kufuatia Upepo Mkali ulioambatana na mvua jana  jioni katika maeneo ya Kwaalamsha, Makadara na Mkele ndani ya Wilaya ya Mjini.
Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema mbali ya mvua na upepo lakini kipindi hichi cha masika pia hukumbwa na miripuko ya maradhi tofauti ya kuambukiza jambo ambalo jamii inapaswa kujihadhari nayo.
Aliwahakikishia wananchi hao kwamba Serikali Kuu kupitia Idara yake ya Maafa ambayo iko chini ya Ofisi yake inaendelea kufanya tathmini na hasara iliyowakumbwa wananchi hao na baadaye iangalie namna ya kusaidia nguvu zitakazowawezesha  kurejea katika  mazingira yao ya awali.
“ Nimekuja na Timu yangu Katibu Mkuu, Mkurugenzi Maafa na timu yake kuanza tathmini na maafa haya na baadaye kuandika ripoti itakayotusaidia sisi Serikalini namna ya kuchukuwa hatua za kukabiliana na maafa hayo yaliyojitokeza “. Alisisitiza Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwapongeza Wananchi mbali mbali waliojitolea nguvu, maarifa na hata hifadhi  ya dharura kwa wenzao  waliopatwa na maafa hayo kufuatia upepo huo wa ghafla.
Alisema kitendo hicho mbali ya kuleta faraja kwa waathirika hao pamoja na Serikali kwa jumla lakini pia kimeongeza upendo na kuimarisha ushirikiano na mshikamano miongoni mwa Wananchi hao.
“ Ukweli nimefarajika sana kusikia kwamba majirani zenu walikuwa pamoja na nyinyi muda wote wa tukio hili. Huu hasa ndio ujirani mwema unaotakiwa kuwemo ndani ya nyoyo za wanaadamu wakati wote “. Alifafanua Balozi Seif.
Wakitoa shukrani zao kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi baadhi ya wananchi hao walioathirika na upepo huo walielezea kufarajika kwao na hatua zilizochukuliwa na majirani zao katika kuwasaidia kukabiliana na maafa hayo.
Nyumba zipatazo Tatu katika Shehia ya Kwaalamsha, Tano Sheria ya Mkele na nyengine kadhaa ambazo bado idadi yake hajijajuilikana katika Shehia ya Makadara zimeathirika kutokana na upepo huo.
Othman Khamis Ame – Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais
Balozi Seif ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar akiangalia jengo la Duka la Mfanyabiashara Khadija Ame Abdulla katika Mtaa wa Kwaalamsha ambalo limeangukiwa na nguzo ya umeme kufuatia upepo mkali uliovuma katika eneo hilo
Balozi Seif ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar akiangalia jengo la Duka la Mfanyabiashara Khadija Ame Abdulla katika Mtaa wa Kwaalamsha ambalo limeangukiwa na nguzo ya umeme kufuatia upepo mkali uliovuma katika eneo hilo
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma  na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma  na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Moja ya kati ya Nyumba  tatu zilizoathirika na upepo mkali uliovuma na kuathiri nyumba mbali mbali katika Mtaa wa Kwaalamsha Mjini Zanzibar
Moja ya kati ya Nyumba tatu zilizoathirika na upepo mkali uliovuma na kuathiri nyumba mbali mbali katika Mtaa wa Kwaalamsha Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma  na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma  na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar
Baadhi ya nyumba zilizoathirika kutokana na upepo Mkali uliovuma na kusababisha hasara kubwa katika Shehia ya Makadara Mjini Zanzibar