Sunday, 5 May 2013

ZIARA YA CHAMA YA MAKAMO MWENYEKITI WA CCM AMBAE PIA NI RAIS WA ZANZIBAR - MKOA WA KASKAZINI UNGUJA


Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Balozi Seif akizungumza na Katibu wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Bibi Catherine Peter Nao wakati wa ziara ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Shein Mkoa Kaskazini Unguja.Kulia yao ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Ndugu Haji Juma Haji.




Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Tifa ya CCM Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo na Makamu Mwenyekiti wa Chama hIcho Zanzibar Dr. Ali Mohammed Sheinn wakati wa ziara yake ya Kichama Mkoa wa Kaskazini Unguja.




Dr. Ali Mohammed Shein na Viongozi wengine wa Chama cha Mapinduzi wakikagua baadhi ya sehemu za Tawi la CCM Kwa Gube Mfenesini akiwa katika ziara ya Kichama ya siku mbili Mkoa wa Kaskazini Unguja.



Mkamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein akitoa kadi kwa wanachama wapya wa CCM hapo tawi la CCM Kwa Gube Mfenesini akiwa katika ziara ya siku mbili ya Kichama Mkoa Kaskazini Unguja.






Wanachama wapya wa CCM Tawi la Kwa Gube wakila kiapo mara baada ya kukabidhiwa kadi zao na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein.




Dr. Shein, Balozi Seif pamoja na Viongozi wengine wakuu wakishangiria hamasa ya Viongozi wa CCM Mkoa Kaskazini Unguja kwenye Mkutano wa Majumuisho wa ziara ya Dr. Shein Mkoani humo.




Baadhi ya Viongozi wa CCM Mkoa Kaskazini Unguja wakiwa katika Kikao cha Kutathmini ziara ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Hicho Zanzibar Dr. Ali Mohd Shein hapo ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya CCM Jimbo la Kitope iliyopo Kinduni Wilaya ya Kaskazini B.






Mzee wa Chama cha Mapinduzi Mkoa Kaskazini Unguja Ali Ameir Mohd akitoa neon la shukrani baada ya kumalizika kwa mkutano wa majumuisho kufuatia ziara ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Sheni Mkoani humo.




Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zanzibar Nd. Vuai Ali Vuai wakibadilisjhana mawazo wakati wa ziara ya siku mbili ya Kichama ya Dr. Shein Mkoa Kaskazini Unguja



Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein akiweka jiwe la msingi la Tawi la CCM Zingwe zingwe wakati wa ziara yake ya Kichama Mkoa wa Kaskazini Unguja.



Picha na Hassan Issa wa
Mwandishi    ni  Othman Khamis    
 VUGA  NEWSROOM - OMPR - ZNZ



No comments:

Post a Comment