Tuesday, 7 May 2013



            SHEREHE ZA KUKABIDHI MCHANGO WA  VIKUNDI  VYA USHIRIKA  WA  WAWANAWAKE 



 WANAUSHIRI wa Vikundi  vya Ushirika vya Wanawake Wilaya ya Chake Chake Pemba wakimsikiliza Mkle wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif, akiwahutubia katika sherehe za kukabidhi mchango uliotolewa na Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, Mama Asha Balozi na Wake wa Wawakilishi na Wabunge wa CCM, makabidhiano hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Makumbusho Chakechake




MKE wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif, akiwahutubia Wanaushirika wa Vikundi vya Wanawake Wilaya ya Chakechake, baada ya kukabidhi misaada iliotolewa na Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, Mama Asha Balozi na Wake wa Wawakilishi na Wabunge kwa ajili ya kuegeze mtaji wa Ushirika wao.



MKE wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif, kushoto akimkabidhi fedha kiongozi wa Kikundi cha Ushirika  cha Wanawake wa Tujiendeleze kwa Maisha Bora Hadia Omar, shiliki laki nne kwa kikundi chao.



WANACHAMA vikundi vya Ushirika vya Wanawake wakishangilia kwa kubeba zawadi zao kumpelekea Mama Asha Balozi .

Picha  na Habari kutoka  
Hassan Issa   na  Othman Khamis
Vuga newsroom
OMPR  - ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment