Tuesday, 14 May 2013

UZINDUZI WA KIWANDA  KIPYA  CHA MAJI   ZANZIBAR


 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza katika uzinduzi wa kiwanda kipya cha maji ya kunywa hapo maeneo huru amani.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifungua pazia kuashiria kukifungua rasmi Kiwanda cjha maji ya Kunywa cha Super Shine Kinachomilikiwa na Kampuni ya Safari yenye Makao Makuu yake Nchini India.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayesimamia Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo Zanzibar Mh. Omar Yussuf Mzee akiwa na akiambatana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kukagua baadhi ya sehemu ya KiwandaKipya  cha Maji ya kunywa kiliopo maeneo ya Viwanda Amani Mjini Zanzibar.

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiangalia baadhi ya mashine za Kiwanda cha maji ya kunywa kiliopo maeneo huru ya Viwanda yaliopo Amani Mjini Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiangalia moja ya sampuli ya chupa ya maji yenye ujazo wa nusu lita ambayo tayari imeshakamilika utayarishaji wake katika kiwanda kipya cha maji ya kunywa kiliopo Maeneo huru Amani.

 Wasanii wa Kikundi cha sanaa Zanzibar wakitoa burdani safi katika hafla ya uzinduzi wa kiwanda kipya cha maji ya kunywa kiliopo amani maeneo huru ya viwanda.


Balozi Seif akiwa pamoja na baadhi ya viongozi  wakishangiria moja ya nyimbo zilizokuwa zikiimbwa na kikundi cha sanaa kwenye hafla ya uzinduzi wa kiwanda kipya cha maji ya kunywa kiliopo maeneo huru ya Viwanda Amani

Mkurugenzi na Mmiliki wa Kampuni ya Safari inayomiliki Kiwanda cha maji ya kunywa kiliopo amani maeneo huru Bibi Mala Kalwan akielezea faraja yake kutokana na ukarimu alioushuhudia Zanzibar wakati akijiandaa kuwekeza Vitega uchumi vyake hapa Zanzibar

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Serikali na wale wa Kampuni ya Safari inayomiliki Kiwanda cha maji ya kunywa  hapo amani eneo huru la Viwanda.
Kulia ya Balozi Seif ni Waziri anayesimamia Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo Mh. Omar Yussuf Mzee, Mkurugenzi Mkuu wa ZIPA Nd Salum Khamis na Mmmoja wa Viongozi wa Kiwanda hicho.Kushoto yake ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Safari inayomiliki Kiwadna hicho Bibi Mala Kalwan na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar Mh. Nassor Ahmed Mazrui.
Habari na Picha Kutoka  HAssan Issa  na  Othman Khamis Vuga  NewsroomAfisi ya  Makamu wa  Pili wa  Rais-Zanzibar



No comments:

Post a Comment