Tuesday, 10 September 2013

KUMBUKUMBU YA WALIOFAKI KWA MELI --ZANZIBAR

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema inaendelea na hatua mbali mbali za kujipanga katika sekta ya usafiri wa baharini ili kuepusha ajali ya meli kuzama isitokee tena  kama ilivyotokea ajali ya Mv.Skagit na MV.Spice islander.

Hayo wameelezwa na Waziri wa Fedha Zanzibar,Mhe.Omar Yussuf Mzee katika kikao cha kumbukumbu ya wahanga walifarika katika ajali hiyo kilichaandaliwa na waandishi wa habari wa maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA).

Alisema Serikali ilichukua juhudi za kuchunguza na kubaini makosa mengi,ambayo yamesababisha ajali ya meli hizo kuzama,hivyo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  imepanga mikati mengi ya kuzuia ajali kama hiyo isitokee tena nchini.

Alisema Serikali ilibaini baadhi ya meli zilifanyiwa maarifa ya kuongezwa ukubwa (Modefication) hivyo Serikali imezisimamisha meli hizo kuendelea kutoa huduma ya usafiri wa baharini.

Mzee alisema Serikali  ilibani kulikua na meli zilikuwa zinafanyakazi kinyume na usajili wake,baada ya kubeba mizigo ilikua na beba abiria,ikiwemo tatizo kuajiri wafanyakazi wasiokuwa na sifa ya utaalam wa kazi hizo.Pia alisema baadhi ya meli zilikua hazina vifaa vya kujihami(life Jacket).

Alisema kutokana msiba mkubwa uliotokea wa Meli hizo mbili kuzama Mv.Skagit na MV.Spice Ilander  Mhe.Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein ameagiza Serikali ichukua hatua ya ununuzi wa meli mpya ya abiria na mizingo.

Alisema katika maagizo ya Mhe.Rais Dkt Shein ameagiza ijengwe meli yenye ubora na yenye usalama ambapo  hatua  za ujenzi wa meli mpya ya abiria imeshaanza kujengwa nchini Korea ya Kusini.

Alielezea Meli hiyo mpya itakuwa na mashini mbili(Engine) ikiwemo na rada,chumba  ambacho kitaweza kufifadhi maiti wa wawili pamoja na chumba cha Daktari atakaekuwa yumo ndani ya meli kila itakapokuwa ipo safarini.

Aidha Mzee alisema Serikali haikukaa kimya imezitaka wamiliki wa vyombo vya usafiri wa baharini vyote viwe na bima ilikua hai(LIVE).Pia alisema Serikali imeshatoa amri meli itakayopakia abiria zaidi  ya uwezo wake isiondoke kinyume na agizo hilo captain na mkuu wa bandari wote watafikishwa katika vyombo vya sheria.

Kwa upande wa wajumbe wa Kikao akizunguza bibi mzuri aliiomba Serikali kuwafikiria jinsi ya kuwasaidia watu walioathirika kisaikolojia kutokana na ajali za meli hizo kuzama.
Alisema kuna watu wameathirika kisaikolojia kwa kupoteza watoto wane kwa wakati mmoja ,baadhi ya wanawake kupoteza mume na watoto.

Kikao hicho kimeandaliwa na Jumuia ya waandishi wa habri za maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA)  ikiwa ni siku ya kumbukumbu ya kuwakumbuka wahanga waliofariki katika ajali ya meli ya Mv.Skagit na Mv.Spice islander iliotokea Septemba 2011 na Julai 2012.
 




No comments:

Post a Comment