Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar imesema inaendelea na hatua mbali mbali za kujipanga katika
sekta ya usafiri wa baharini ili kuepusha ajali ya meli kuzama isitokee tena kama ilivyotokea ajali ya Mv.Skagit na
MV.Spice islander.
Hayo
wameelezwa na Waziri wa Fedha Zanzibar,Mhe.Omar Yussuf Mzee katika kikao cha
kumbukumbu ya wahanga walifarika katika ajali hiyo kilichaandaliwa na waandishi
wa habari wa maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA).
Alisema Serikali
ilichukua juhudi za kuchunguza na kubaini makosa mengi,ambayo yamesababisha
ajali ya meli hizo kuzama,hivyo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepanga mikati mengi ya kuzuia ajali kama
hiyo isitokee tena nchini.
Alisema Serikali ilibaini baadhi ya meli zilifanyiwa maarifa ya kuongezwa ukubwa
(Modefication) hivyo Serikali imezisimamisha meli hizo kuendelea kutoa huduma
ya usafiri wa baharini.
Mzee alisema Serikali
ilibani kulikua na meli zilikuwa zinafanyakazi kinyume na usajili wake,baada
ya kubeba mizigo ilikua na beba abiria,ikiwemo tatizo kuajiri wafanyakazi
wasiokuwa na sifa ya utaalam wa kazi hizo.Pia alisema baadhi ya meli zilikua hazina
vifaa vya kujihami(life Jacket).
Alisema kutokana msiba mkubwa uliotokea wa Meli hizo mbili
kuzama Mv.Skagit na MV.Spice Ilander
Mhe.Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein ameagiza Serikali ichukua
hatua ya ununuzi wa meli mpya ya abiria na mizingo.
Alisema katika maagizo ya Mhe.Rais Dkt Shein ameagiza ijengwe
meli yenye ubora na yenye usalama ambapo hatua za
ujenzi wa meli mpya ya abiria imeshaanza kujengwa nchini Korea ya Kusini.
Alielezea Meli hiyo mpya itakuwa na mashini mbili(Engine)
ikiwemo na rada,chumba ambacho kitaweza
kufifadhi maiti wa wawili pamoja na chumba cha Daktari atakaekuwa yumo ndani ya
meli kila itakapokuwa ipo safarini.
Aidha Mzee alisema Serikali haikukaa kimya imezitaka wamiliki
wa vyombo vya usafiri wa baharini vyote viwe na bima ilikua hai(LIVE).Pia
alisema Serikali imeshatoa amri meli itakayopakia abiria zaidi ya uwezo wake isiondoke kinyume na agizo hilo
captain na mkuu wa bandari wote watafikishwa katika vyombo vya sheria.
Kwa upande wa wajumbe wa Kikao akizunguza bibi mzuri aliiomba
Serikali kuwafikiria jinsi ya kuwasaidia watu walioathirika kisaikolojia
kutokana na ajali za meli hizo kuzama.
Alisema kuna watu wameathirika kisaikolojia kwa kupoteza
watoto wane kwa wakati mmoja ,baadhi ya wanawake kupoteza mume na watoto.
Kikao hicho kimeandaliwa na Jumuia ya waandishi wa habri za
maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) ikiwa ni
siku ya kumbukumbu ya kuwakumbuka wahanga waliofariki katika ajali ya meli ya
Mv.Skagit na Mv.Spice islander iliotokea Septemba 2011 na Julai 2012.
No comments:
Post a Comment