Sunday, 6 October 2013

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Bibi Ingunn Klirpsvik Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar
























Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Bibi Ingunn Klirpsvik  Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar ambapo walipata wasaa wa kubadilishana mawazo juu ya uhusiano wa mataifa yao mawili.

Serikaliya Mapinduzi ya Zanzibar imeshauriwa kujifunza kupitia Mataifa, Taasisi na Mshirika ya Kimataifa katika mpango wake iliyolenga wa kuelekea kwenye mradi mpya wa uzalishaji wa Mafuta.
Balozi wa Norway Nchini Tanzania Bibi Ingunn Klirpsvik alitoa ushauri huo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Balozi Ingunn alisema hatua hiyo ya tahadhari inayofaa kuchukuliwa na Zanzibar inaweza kuwa mwanzo mzuri wa kuingia katika mradi huo mpya wa Kiuchumi  kwenye muelekeo wa mafanikio makubwa.
Balozi huyo wa Norway Nchini Tanzania alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Norway wakati wote iko tayari kutumia ujuzi  wake mkubwa katika masuala ya Mafuta kuisaidia Zanzibar kitaalamu ili ifanikiwe katika malengo iliyojipangia katika kuendesha mradi huo.
Alifahamisha kwamba Nch hiyo imekuwa mshirika mkubwa wa Tanzania na Zanzibar kwa ujumla katika kuunga mkono harakati za kiuchumi na ustawi wa Jamii wa wananchi walio wengi Nchini.
“ Tumekuwa na ushirikiano na uhusiano wa muda mrefu katik a pande zetu hizi mbili unaolenga kustawisha harakati za kijamii na uchumi kwa wananchi walio wengi “. Alisisitiza Balozi huyo wa Norway Nchini Tanzania Bibi Ingunn  Klirpsvik.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameishukuru Serikali ya Norway kwa juhudi zake za kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika maendeleo hasa uungaji mkono katika miradi ya miundo mbinu ya Kiuchumi.
Akizungumzia suala la amani ambalo linaonekana kuiteteresha pembe ya Bara la Afrika Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema Tanzania imelazimika kuchukuwa tahadhari ili kudhibiti wimbi hili linaloonekana kulikumba eneo hilo.
Balozi Seif alisema Serikali aya Tanzania  iko makini katika kufuatilia wageni wasio na mfumo sahihi wa kuishi ndani ya ardhi ya Tanzania na jitihada zinachukuliwa katika kuratibu wageni walioamua kuishi Nchini kupitia Sheria na taratibu zilizopo za Kitaifa na Kimataifa.
“ Tanzania imelazimika kuwa na tahadhari katika masuala  ya ulinzi wa amani ili kujaribu kuzuia au kudhibiti uasi ama ubabe unaoweza kufanywa na watu au vikundi vinavyopenda kuichezea amani “. Alisisitiza Balozi Seif.
Kuhusu suala la mchakato wa kuelea kwenye Katiba mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimueleza Balozi huyo wa Norway Nchini Tanzania Bibi Ingunn kwamba mabaraza ya Katiba ya Wilaya  yamekamilisha vyema mijadala yao.
Balozi Seif alisema hatua hiyo ndio iliyopelekea Bunge la Jamuhuri ya Muungano kujadili Marekebisho ya  sheria ya Katiba na kuipitisha ili kuundwa kwa Bunge la Katiba litakalojadili na  kuidhinsha i   kupigwa kwa kura ya maoni hapo baadaye ili kuamilisha mchakato mzima wa kupata katiba mpya.
Balozi Seif aliendelea kusisitiza kwamba Zanzibar imeshirikishwa kikamilifu katika mchakato mzima wa kujadili katiba hiyo kuanzia msingi licha ya malalamiko na shutuma zinazoendelea kutolewa na upande wa upinzani kwamba Zanzibar haikushirikishwa.

No comments:

Post a Comment